Balaa: Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey alitolewa nje kwa kadi nyekundu katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Besiktas
ASERNAL wamelazimisha suluhu pacha ya bila kufungana na Besiktas ya Uturuki katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa ligi ya mabaingwa barani Ulaya uliopigwa jana usiku katika dimba la Ataturk Stadium
Kutoka sekunde za mwanzo, almanusura Demba Ba afunge bao lakini mpira aliopiga wa adhabu ndogo uligonga mwamba na ilionekana kuwa ni mechi ambayo ingekuw ana magoli mengi.
Lakini Aaron Ramsey naye aliwakosa Waturuki hao baada ya kupiga shuti lililogonga mwamba.
Kadi nyekundu ya Aaron Ramsey aliyopata dakika za majeruhi kufuatia kuoneshwa kadi mbili za njano aliwahuzunisha zaidi Asernal kutokana na ukweli kuwa anahitajika sana katika mchezo wa marudiano ndani ya dimba la Emitarates.
Besiktas, na Ba wameonekana kuwa na nia ya kuwaonesha Chelsea kuwa walifanya makosa kumuuza mshambuliaji huyo kwani alionesha kiwango kizuri.
Ili kusonga mbele, Asernal wanahitaji ushindi wa bao 1-0 tu mjini London jumanne ijayo.
Ramsey (kushoto) alioneshwa kadi ya pili ya njano baada ya kumuangusha mchezaji wa Besiktas, Oguzhan Ozyakup (kulia)
Amri ya 'jaji': Mwamuzi wa Serbia, Milorad Mazic (kushoto) hakuwa na jinsi zaidi kutoa kadi nyekundu kwa Ramsey baada ya kufanya madhambi.

Ramsey akitoka nje ya uwanja wa Ataturk Stadium

Refa vipi bwana, mbona tunaharibiana kazi?: Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger hakuamini kilichotokea uwanjani baada ya kuona nyota wake tegemeo ametolewa kwa kadi nyekundu
0 comments:
Post a Comment