


Japokuwa kuna wasiwasi kama nyota huyo atacheza mechi ya ufunguzi ya kundi D dhidi ya Costa Rica juni 14 kwenye uwanja wa Estadio Castelao, Suarez anatazamiwa kuwa fiti kabla ya mashindano kuanza.
"Nawashukuru wote kwa sapoti yenu," aliwaambia La Ovacion akiwa nchini kwake Uruguay.
"Nitajitahidi na kufanya maandalizi kwa bidii siku zijazo ili kuwa fiti kwa asilimia 100 na kuwasaidia wachezaji wenzangu".
Hizo ni habari njema kwa taifa hilo la America kusini ambalo lilifika hatua ya nusu fainali ya michuano iliyopita ya kombe la dunia nchini Afrika kusini.
Mama yake Suarez, Sandra Diaz alifurahi baada ya zoezi za upasuaji kufanikiwa.
Alisema: ‘upasuaji umekamilika na tunamshukuru Mungu kila kitu kimekwenda vizuri. Tatizo la Luis halikuwa kubwa sana kama tulivyodhani"

0 comments:
Post a Comment