
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Imechapishwa Mei 27, 2014, saa 8:52 asubuhi
TIMU ya Taifa ya Tanzania chini ya kocha mkuu,
Mholanzi, Mart Nooij inatarajia kujipima ubavu katika mechi ya kimataifa ya kirafiki
jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) kuanzia
majira ya saa 11:00 jioni.
Taifa Stars iliyopiga kambi yake mjini Tukuyu jijini
Mbeya inatarajia kuwasili asuhubi hii majira ya saa 4:00 katika uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ndege ya Air Tanzania.
Wapinzani wa Taifa stars tayari wapo jijini Dar es
salaam kwa ajili ya mechi hiyo muhimu kwa makocha kuangalia uimara wa timu zao kabla ya kwenda
kucheza mechi za mashindano.
Stars na Malawi wanakutana kwa mara ya pili ndani ya
mwezi mmoja kwani mei 4 mwaka huu walipambana tena katika uwanja wa Sokoine
jijini Mbeya na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana.
Mechi hii itatumika na kocha mkuu wa Taifa stars,
Nooij, kuangalia kama kuna maboresho katika kikosi chake kinachojiandaa na
mechi ya marudiano dhidi ya Zimbabwe mjini Harare.
Mechi ya kwanza jijini Dar es salaam ambayo Stars
ilishinda kwa bao 1-0 la John Bocco `Adebayor`, safu ya kiungo ilionekana
kupwaya sana, hivyo leo hii itakuwa nafasi ya kocha kuona kama viungo wake
wameimarika.
Pia safu ya ushambuliaji ilionekana kukosa nafasi
muhimu za kufunga na kwa muda wote walipokuwa Tukuyu, Nooij alikuwa anahangaika
kunoa makali ya washambuliaji wake.
Malawi (Flames) inayonolewa na mchezaji wake wa zamani
Young Chidmozi nayo itakuwa inacheza mechi ya mwisho ya majaribio kabla ya
kwenda N’djamena kuikabili Chad.
Shirkisho la soka Tanzania, TFF kupitia kwa Afisa
habari wake, Boniface Wambura Mgoyo limewataka watanzania kujitokeza kwa wingi
kuishangilia timu yao ambayo kwa sasa inajengwa upya.
Wambura alitaja kiingilio katika mechi hiyo kuwa kitakuwa
sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa upande wa VIP B na
C kiingilio kitakuwa sh. 10,000 wakati kwa VIP A itakuwa ni sh. 20,000.
0 comments:
Post a Comment