Saturday, May 31, 2014


http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/07/Baadhi-ya-wachezaji-Kikosi-cha-Timu-ya-Taifa-Uganda.jpg
Uganda The Cranes wana kibarua cha kufuta kipigo cha mabao 2-1 katika mechi ya kwanza

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 31, 2014, saa 5: 02 asubuhi

MATAIFA mbalimbali barani Afrika leo yanashuka dimbani kusaka nafasi ya kupangwa katika hatua ya makundi kuwania kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika, AFCON 2015 nchini Morocco.
Jana mechi mbili zilipigwa ambapo Kenya walilazimisha sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya Comoros na kufanikiwa kusonga mbele kutokana na ushindi wa bao 1-0 walioupata mjini Nairobi.
Sudan kusini waliofungwa mabao 5-0 na Msumbiji mjini Maputo, jana waliwakaribisha wapinzani wao nyumbani na kutoka suluhu ya bila kufungana.
Kwa matokeo hayo, Msumbiji wamesonga mbele na wanasubiri mshindi wa mechi ya Taifa stars na Zimbabwe ili kuumana naye katika hatua ya mwisho kuwania kupangwa hatua ya makundi.
Mechi nyingine zinatarajia kuendelea leo katika nchi mbalimbali barani Afrika.
Timu ya Taifa ya Rwanda iliyotoka suluhu ya bila kufungana nyumbani mjini Kigali dhidi ya Libya, leo wanacheza mechi ya marudiano ugenini  mjini Tripoli na wenyeji wao.
Uganda The Cranes wanawakaribisha Madagascar mjini Kampala. Mechi ya kwanza Uganda walifungwa mabao 2-1.
Guinea Bissau wanachuana na Jamhuri ya Afrika ya Kati. Mechi ya kwanza timu hizo zilitoka suluhu pacha ya bila kufungana.
Sierra Leone wakiwa na  kumbukumbu ya kutoka sare ya bao 1-1 ugenini , wanaikaribisha katika mechi ya marudiano, Jamhuri ya Swaziland.
Mechi nyingine zitapigwa kesho juni 1 ambapo timu taifa ya Tanzania, Taifa stars itakabiliana na wenyeji wao, Zimbabwe, mjini Harare.
 10357474_634079413340945_8148690486284095511_n
Taifa Stars walioripotiwa kufanyiwa hujuma hapo jana kwa kufungiwa Hoteli wanayoishi mjini Harare, wanahitaji sare ya aina yoyote au ushindi ili kusonga mbele. Hii inatokana na ushindi wa bao 1-0 walioupata uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Lesotho waliofungwa bao 1-0 ugenini, watawakaribisha wapinzani wao Liberia katika mechi ya marudiano.
Nao Botswana waliotoka suluhu mjini Bujumbura, kesho watawakaribisha Burundi nyumbani kwao.
Congo yenye kumbukumbu ya kuchapwa bao 1-0 na Namibia, kesho itakuwa nyumbani kulipa kisasi.
Katika mechi nyingine, Benin waliotoka suluhu mechi ya kwanza, watakuwa nyumbani kuvaana na Sao Tome.
Chadi waliofungwa mabao 2-0 na Malawi, kesho watakuwa kwenye kibarua kigumu nyumbani kuhitaji kufuta matokoe hayo.
Guinea ya Ikweta iliyofungwa bao 1-0 ugenini, kesho itahitaji ushindi nyumbani katika mechi ya marudiano na Mauritania.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video