Wednesday, May 28, 2014



Geoffrey-Nyange-Kaburu
Na Baraka Mbolembole
REJEA kutoka katika makala niliyoandika wiki iliyopita ambayo ilikuwa na kichwa cha habari; ‘ NAFASI YA MAKAMU WA RAIS SIMBA SC HAINA MTU SAHIHI’. Mmoja wa wagombea wanaowania kiti hicho katika uchaguzi ujao wa klabu ya Simba Geofrey Nyange Kaburu, juzi alitoa ufafanuzi kuhusiana na yale ambayo nilikuwa nimeandika dhidi yake. Katika makala hiyo niliandika kuwa, Kaburu anarudi Simba kufanya nini wakati nyuma yake ni mmoja wa viongozi ambao wachezaji wengi walikuwa wakimlaumu kwa kutowathamini, kuwajali nap engine kushindwa kuwalipa pesa zao.
Sehemu ya makala ile niliandika kwamba;  ‘Kwa, mfano, mimi ningewaambia, Itangare na Kaburu wakajifunze kwanza jinsi ya kuunganisha mahusiano ya kiutawala kati ya kiongozi wa chini na yule wa nafasi ya juu. Wote hawa walishindwa kwenda sambamba na mwenyekiti anayemaliza muda wake, Mh. Aden Rage. Nakumbuka kuna wachezaji wengi waliwahi kuniambia kuhusu kutothaminiwa, kunyanyaswa katika malipo, na kudharauliwa na makamu huyo mwenyekiti wa zamani aliyejiuzulu katika utawala unaomaliza muda wake’
Akizungumza kwa utulivu na kujiamini, makamu huyo mwenyekiti wa zamani aliyejiuluzu baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka isiyozidi miwili, amefunguka mengi. Ni kwanini aliamua kujiuzulu katika nafasi hiyo huku akitumia muda mwingi kuwazungumzia wachezaji wa klabu hiyo katika mambo mbalimbali ambayo wa,ekuwa wakilalamikia nje ya klabu.
KABURU; Siwagawi wachezaji, umeniandika kwa nia ya kunichafua. Hukuwahi kuniuliza kwa nini nilijiuzulu katika nafasi yangu ndani ya Simba. Nimeongoza pale kwa miaka miwili tena kwa mafanikio makubwa. Makala yako haikunitendea haki hasa mimi. Kwa sababu umesema kuwa uliongea na wachezaji na wamekuambi vitu fulani. Ndiyo, inawezekana ni kweli hayo wanayokuwa wakisema, au yasiwe mambo ya kweli, ama pengine inawezekana ikawa ni katika utaratibu wa klabu. Ungepaswa kuniuliza kwanza kabla ya kuandika ili kuwe na mizani katika makala yako, ila hukufanya hivyo. Umeandika kwa nia ya kunichafua hasa kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu wa klabu.
SWALI;  Kama kuna kitu kibaya nimekiandika, naomba samahani, ila huo ndiyo ukweli kutoka kwa wachezaji wenu. Si mchezaji mmoja anayelalamika kuhusu hayo, watu wanne hadi watano nafikiri wanatosha kunipatia hali halisi.
 KABURU; Inawezekana wakati mimi nikiwa kiongozi kuna mchezaji akawa anadai, ila hapa ieleweke kuwa hakuwa anamdai, Kaburu, anaidai klabu. Mchezaji  anaweza kuwa na mikataba yake lakini akishindwa kuendana na mahitaji ya Mwalimu hivyo hapo ni lazima ufanye mabadiliko. Kama, Mwalimu anakuambia ' fulani simuhitaji'. Kama viongozi ni kuchukua uamua wa kumuondoa na kuleta mwingine ambayo anahitajika.
Tuna muandalia utaratibu wa kumlipa, na anaweza kulipwa wakati huo kidogo au akaambiwa atalipwa nyingine baadae. Mfano, wachezaji wengi wa Simba ukisoma mikataba yao inasema kabisa, labda mchezaji anasajiliwa kwa millioni kumi, hupewa millioni tano wakati akisaini na katika mwaka wa pili anapewa tena millioni tano. Kwa hiyo mtu  anaweza kusema anadai pesa ila kuna vitu vingi katikati mchezaji akawa havijui vizuri, au anaongea kwa nia tofauti.
SWALI, Je hakuna hali hiyo?
KABURU; Uongozi ni ' jalala', mimi wakati naingia pale kweli nilikuta utaratibu wa wachezaji kulipwa pesa mkononi. Niliondoa hali hiyo na hadi sasa wachezaji wanalipwa moja kwa moja kwa kuingiziwa pesa katika akaunti zao.
SWALI, Pesa ya mishahara inatoka wapi na nani anayehusika na kuwalipa wachezaji?
 KABURU; Pesa ya mishahara inatoka kwa mdhamini, na anayefanya kazi hiyo ni Mtendaji mkuu wa klabu.
SWALI; Kwa nini baadhi ya wachezaji wanakunyoshea wewe vidole vya lawama?
 KABURU; Hakuna mchezaji aliyotoka chini ambaye sikumsaidia, ila msaada wangu wote unakuwa na maana mchezaji anatakiwa naye kuisaidia klabu. Kama mchezaji anasaidiwa naye hatoi msaada kwa klabu utafanya nini? Mwalimu akisema fulani simuhitaji, mimi nifanyaje?.Ripoti ya Mwalimu inakuja katika kamati ya utendaji, maamuzi yakifanyika baada ya kuijadili tunakuwa wazi, mchezaji husika anaambiwa wazi kuwa ameshindwa kufikia malengo ya Mwalimu.
 Mfano, ripoti ya Z. Logarusic inaoneshawachezaji wengi wanatakiwa kuvunjiwa mikataba yao kwa sababu hawajafikia malengo.  Si mchezaji mmoja au wawili ni wengi. Hii ni inshu' serious', itabidi wengine tuwapunguze kwa kuwapeleka kwa mikopo katika timu nyingine kwa kuwa hatuwezi kuvunja mikataba ya wachezaji wote. Uamuzi huo unapofika kwa mchezaji anaona anawekewa zengwe na Kaburu. Mpira ni ugaidi. Unamfahamu vizuri, Ferguson ( Sir Alex)?. Hacheki na mtu anapoamua kufanya mabadiliko, ni mtu mwenye roho mbaya. Kwenye soka kila mtu anatakiwa kufanya kazi yake ipasavyo, ndiyo utaratibu uliopo kila mahali.
Kwa vile mchezaji hajui atalalamika. Tazama, mchezaji gani ambaye Mwalimu, Loga hakumpatia nafasi?. Wote amewapatia nafasi ila wameshindwa. Leo hii, ukiwaambia wachezaji kama, Mwombeki ( Betram), Pazzi ( Zahoro) au Christophe ( Edward) waende mahali kwa mkopo ili wapate nafasi ya kucheza watakataa, ila ni nafasi nzuri ya wao kujiimarisha kimpira. Hawa ni mfano tu, lakini wapo wengi ambao ukichukua maamuzi kama hayo wanajenga chuki na kuona wanaonewa au hawatendewi haki.
SWALI; Kumekuwa na madai kuwa viongozi kuwajali zaidi wachezaji fulani wanaotajwa ni nyota katika timu na kuwapuuza wale wengine ambao ukitazama kwa umakini utaona mchago wao pia ni mkubwa. Wewe ni mmoja wa viongozi ambao wanalalamikiwa sana kuhusu hilo, unasemaje?
 KABURU; Nataka nikupe mfano mmoja, Emmanuel Okwi, ni watu wangapi ambao walikuwa wakimzunguka mara baada ya kumalizika kwa mchezo?. Ni wengi, je, ni kwanini wamfuate yeye?. Kiwango chake cha uwanjani kinawavutia wengi hivyo wengine wanaamua kumpa asante kwa kazi yake nzuri, hivyo mchezaji mwingine akiona hivyo roho inamuuma. Ukimwambia naye afanye jitahada mazoezi ili awe bora zaidi hataki.
Wewe ndiye ungekuwa kiongozi utafanya nini?. Kwenye mpira kila mchezaji atakula kutokana na urefu wa kamba yake, ili ni lazima Watanzania walijue. Mwanzo kila mchezaji alikuwa akipewa kiasi sawa na mwenzake katika kila mgao, lakini, Mwalimu  akasema, hapana mchezaji atakaye fanya vizuri apewe kiasi cha juu zaidi na yule ambaye atashindwa apewe kidogo ama huenda asipewe kabisa. Anayefanya kazi zaidi, ndiye atakayekula zaidi.
SWALI; Kwa nini ulijiuzulu katika nafasi yako ya umakamu mwenyekiti?.
KABURU; Nilijiuzulu Simba kwa sababu nyingi, lakini kubwa ni suala la katiba. Nilijiuzulu kwa kuwa sikufurahishwa na jinsi ambavyo sisi kama uongozi tulivyokuwa na mtazamo tofauti kuhusu mambo ya usajili wa wachezaji. Niliwaambia wenzangu mpango wa kuwaondoa wachezaji wote wakongwe haukuwa sahihi.
Wao walitaka tuwapandishe vijana wote wa timu B, ili kuchukua nafasi za wachezaji wazoefu. Nilikataa kuhusu hilo na nikasisitiza kuwa tutafanya kosa, kwa kuwa timu ilikuwa ikihitaji matokeo zaidi kwa sasa. Nikapendekeza tuwe tunapandisha kijana mmoja mmoja kila msimu katika kikosi cha kwanza. Mfano, Shomari Kapombe aliingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza mwaka juzi, wakafuata kina, Ramadhani Singano, Haruna Chanongo, Jonas Mkude.
 Kuwapandisha wote kwa pamoja ilikuwa na maana ya kujitoa katika ushindani. Mimi ndiye niliyeitengeza timu ya U20, hakuna kiongozi aliyekuwa na mpango na timu hiyo. Niliamua kumsomesha, Suleimani Matolaili aweze kunisaidia katika hilo. Nimemsomesha, Singano tangu kitado cha kwanza hadi cha nne, nimewasaidia vijana wengi, hatukuwa na mishahara lakini nilikuwa na mawazo kuwa baada ya miaka minne nitagombea uongozi na vijana hao watanibeba.
SWALI; Kwa nini ulipingana mpango huo wa kuwapandisha wachezaji vijana?
 KABURU; Lengo letu kubwa ilikuwa ni kusajili wachezaji wazawa, huku tukilenga kuwasaini vijana wa timu B, ili klabu isiwe na wasiwasi wa kuhujumiwa kwani mara nyingi wachezaji wa ndani husemwa kuwa wanajihusisha na uuzwaji wa mechi hivyo mpango wa timu  B, ulitakiwa kutazamwa lakini si haraka vile. Wakati naingia katika uongozi wale vijana walikuwa pamoja kwa miaka mitatu, na mawazo yangu ilikuwa ni kuwaingiza kikosini mmoja mmoja. Mimi sikukubaliana na wenzangu timu yote ipandishwe kwa sababu hawakuwa na uzoefu wa ligi.
 Huwezi kumpandisha mchezaji kinda anayecheza mechi nne kwa mwaka. Nikatoa mawazo kuwa baadhi yao tuwapeleke kwa mkopo katika timu nyingine ili wapate uzoefu. Kamati ya utendaji yote ilikataa, lakini wamefeli. Kuuza mchezaji bila kufikiria ni mchezaji gani utamsajili kama mbadala wake lazima utafeli.
SWALI; Unamaanisha nini?
KABURU; Mimi nilikataa, Okwi asiuzwe. Nakumbuka nilimwambia ' mwenyekiti usimuuze mchezaji huyo', akalazimisha na wenzake wakamuuza bila pesa. Kama msaidizi wa mwenyekiti maana yake nigombane na mwenyekiti ili timu iende katika mgogoro. Kipi bora?.Cha kufanya nikaamua kujiuzulu.
SWALI; Simba haikufanikiwa sana katika michezo ya kimataifa, tatizo lilikuwa ni nini?
 KABURU; Mtu aliyetuangusha ni Rage, mwaka juzi tulifika hadi hatua ya 16 bora ya kombe la Shirikisho. Alienda Sudan bila kuwa na wachezaji muhimu. Nilimwambia ni lazimatwende kule na plan tofauti akakataa. Akaichukua timu akaenda nayo, nikamwambia nenda. Hivi katika mchezo wa kimataifa unaweza kwenda uwanjani bila kuwa na mshambuliaji? Alimuacha, Okwi nyumbani kwa sababu tu ya mchezaji kutaka mkataba mzuri zaidi baada ya ule wa awali kumalizika. Ilikuwa kosa lake. ( kumbuka Simba il)
SWALIL Nini kinafuata sasa?
Kaburu; Hakuna kiongozi ambaye amefanya mambo ambayo mimi nimefanya, napenda sana kukosolewa, lakini napokuwa naonewa huwa sijisikii vizuri kwa sababu nimejitoa sana kwa klabu hii. Nimeingia TFF, katika kamati ya LIgi ili kuzisadia klabu kuboresha timu zao za vijana ambazo ndiyo msingi mkubwa. Kuanzia msimu ujao tuna mpango kuwa timu zote za vijana zicheze katika ligi ya  mkoa na zikiweza zinapanda daraja la pili, hadi la kwanza hazitaruhusiwa kucheza ligi kuu kwa kuwa  huwezi kuzichezesha timu mbili katika daraja moja. Hivyo ndivyo wanavyofanya, Hispania, Ujerumani na kwingineko duniani.
Mimi ni mtu wa vitendo, mimi ni mtu wa watu. Tangu nimeondoka katika uongozi Simba haijashinda taji lolote. Kwa nini> Sababu kubwa ni kwamba Simba inahitaji pesa kwanza, usajili mzuri, kufanya maandalizi ya uhakika ya ligi. Timu inaposhinda watu watakuja uwanjani, na klabu itapata pesa . Kuuza wachezaji ilikuwa ni moja kati ya mipango yangu. Kwamba kila mwaka tunauza mchezaji mmoja na kutumia pesa hiyo kusajili wachezaji wengine, watatu hadi wanne wenye uwezo pia .Kwa nini? Ili timu ipate pesa na iweze kujiendesha. Sijisifii, ila nilikuwa na maarifa , Kwanza, nilikuwa nikiwasaini wachezaji wazuri na kutengeneza timu bora kwa kufuata maagizo ya Mwalimu.
SWALI; Umejifunza wapi?
KABURU; Mwaka 2005 nilikwenda na Simba nchini Nigeria wakati tukienda kucheza na timu ya Enyimba, nilipofika kule  nilikutana na rais wa timu hiyo naye akaniambia kuwa ‘ hatua wachezaji’ kwa maana kuwa wachezaji wetu hawakuwa wameandaliwa katika misingi ya uchezaji. Akanielekeza jinsi ya kuandaa timu, nan i huko ndipo nilikopatia wazo la kuja kuanzisha timu B ya Simba. Nakumbuka nilijenga mahusiano mazuri na rais wa Enyimba na kuna wakati akatupatia bure wachezaji Emeh Ezechukwu na Orgi Obinna. Nimetembea, Ujerumani, Hispania, Ufaransa nan chi nyingine za Ulaya na Afrika kote huko nilienda kwa nia ya kujifunza kuhusu uendeshaji wa mambo ya mpira.
Nashukuru, sana kiongozi kwa kutoa ufafanuzi mzuri kuhusu hoja yangu.
KABURU; Asante pia, ila wakati mwingine ni lazima utafute wahusika kwanza na kuandika. Sina tatizo na wewe ila makala yako ilikuwa na lengo la kunichafua .
0714 08 43 08

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video