Thursday, May 29, 2014

 http://4.bp.blogspot.com/-B_8N4wTiv4w/Un93BcxS2uI/AAAAAAAADiw/OVCaTLamizo/s640/u20.jpg
Na Mwandishi Wetu, Tanga
MABINGWA wa Kombe la Uhai ambalo hushirikisha wachezaji wanaotumikia vikosi vya pili kwenye timu zinazoshiriki ligi kuu soka Tanzania bara,Coastal Union U-20 Jumapili wiki  hii wanatarajiwa kufanya ziara ya kimichezo Tarafa ya Maramba wilayani Mkinga .
Timu hiyo itacheza mchezo mmoja wa kirafiki na Viva Dynamo ya Maramba lengo likiwa kujenga undugu na kuwapa burudani wapenzi wa soka wilaya pamoja na kuwapa fursa kuiona timu hiyo ikicheza kwenye viwanja vyao vya nyumbani.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa soka JKT Maramba unaomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa wilayani humo ambapo msafara huo utaongozwa na mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union,Hemed Aurora wakiwemo viongozi wengine.
Akizungumza na waandishi wa habari ,Ofisa Habari wa timu ya Coastal Union,Oscar Assenga alisema ziara hiyo ni miongoni mwa mikakati ya timu hiyo kuzunguka wilaya zote za mkoa wa Tanga kwa ajili ya maandalizi  ya msimu mpya wa Ligi kuu pamoja na mashindano ya Rolling Stone ambayo hufanyika kila mwaka.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video