Saturday, May 31, 2014


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 31, 2014, saa 10: 12 jioni

WENYEJI wa michuano ya CECAFA Nile Basin Cup, Al-Merreikh ya Sudan wametupwa nje ya michuano hiyo kwa penati 3-2 baada ya dakika 90 za kawaida kumalizika kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Academie Tchite ya Burundi.
Merreikh ndio walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza dakika ya 4 kupitia kwa Agab Ramadan, lakini dakika ya 22 Academie wakasawazisha kupitia kwa Manishimwe Alain na matokeo hayo yalidumu mpaka dakika ya 90 na mshindi kupatikana kwa mikwaju ya penati.
Wachezaji wa Al-Merreikh waliokosa penati ni Amir Kamal, Wawa Pascal na Tia Togbi Olivier. Waliofunga ni Only Sadjo Haman na Elbasha Ahmed.
Vijana wa Academie waliofunga penati jana ni Ngando Omar, Barampanze Shaban na Manishimwe Alain. Mlinda mlango wa Academie Sonzera Anslem ndiye alikuwa nyota wa mchezo huo.
Mchezo wa mapema wa robo fainali uliwakutanisha AFC Leopard ya Kenya na Defence kutoka nchini Ethiopia.
Mchezo huo ulimalizika kwa Leopard kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 na kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hii mipya katika ukanda huu wa Afrika mashariki.
Kamati ya mashindano ya CECAFA Nile Basin Cup imekutana leo asubuhi katika Hoteli ya Grand Holiday Villa mjini Khartoum, imehamishia mechi zote kwenda uwanja wa Khartoum.
Mechi za leo za robo fainali kati ya Victoria University dhidi ya Mbeya City fc na nyingine ya Ahly-Shandy na Malakia fc zilipangwa kufanyika kwenye uwanja wa Al-Merreikh.
Lakini barua iliyotumwa kwa klabu zote na katibu mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye anasema mabadiliko hayo yanatakiwa kufanyiwa kazi mara moja.
“Kutokana na majukumu mengine ya uwanja wa Al-Merreikh, ninataarifu kuwa mechi zote zilizosalia leo jumamosi, zimehamishiwa uwanja wa Khartoum. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza”. Ilisomeka barua ya Musonye.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video