
Matumaini bado yapo: Van Persie akifunga bao la kwanza la kuongoza usiku wa jana Old Trafford
Alijaribu kuokoa: Mlinda Mlango Roberto alikwenda njia sahihi, lakini shuti laVan Persie lilikuwa na nguvu zaidi 
Presha kubwa: Van Persie akijaribu kutumia vyema pasi aliyopewa na Wayne Rooney

Penati! : mholanzi huyo aliangushwa na Jose Holebas, baada ya hapo mwamuzi akawapa Man United penati

Mambo magumu: Patrice Evra akijaribu kumiliki mpira, huku Leandro Salino akikomaa naye

Huniwezi mbwana mdogo!: Giggs (kushoto) akichuana na mchezaji wa Olympiakos, Hernan Perez

Umetunyima?: United walilalamikia kunyimwa penati nyingine kipindi cha kwanza kufuatia Valencia kuangushwa eneo la hatari na Maniatis

Ni shidaa: Beki wa Olympiakos, Kostas Manolas alicheza bega kwa bega dhidi ya Danny Welbeck
Hapa vita tu: Antonio Valencia, akipewa shughuli na Alejandro Dominguez
Heheheh!!: Antonio Valencia United akipigwa kichwa kwenye jicho na Joel Campbell wa Olympiakos

Aling`ara: Antonio Valencia baada ya kupata mshikeli kwenye jicho kufuati kupigwa kichwa na Joel Campbell

Kutoka nyuma: Beki wa United, Patrice Evra akichuana na Hernan Perez wa Olympiacos

Mtu aliyefanya yote: Sir Alex Ferguson alikuwepo jana usiku kuhakikisha mambo yanakwenda sawa
Picha na Sportsmail


0 comments:
Post a Comment