Saturday, March 15, 2014

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam


0712461976 au 0764302956


SASA kimeeleweka Simba Sc na huenda  kiu ya wanachama wake imekatwa baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji  kilichomalizika mchana wa leo jijini Dar es Salaam, kupanga Mei 4,mwaka huu iwe tarahe ya Uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo.


Afisa Habari wa Simba SC, Asha Muhaji  ameuambia mtandao huu kuwa kikao hicho pia kimeunda Kamati ya Uchaguzi.


Alisema Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ni mwanasheria mashuhuri, Damas Ndumbaro na Makamu wake ni Salum Madenge.


Wajumbe wengine ni Issa Batenga ambaye ni Katibu, Khalid Kamguna Katibu Msaidizi na Wajumbe Kassim Dewji, Juma Simba na Amin Bakhresa.


Jambo lingine ambalo Asha alieleza ni kuwa kesho, Simba SC inatarajiwa kufanya mkutano wa wanachama wake kwa ajili ya kuifanyia marekebisho Katiba yao kwa maagizo ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).


Afisa habari huyo aliwaomba wanachama hai wa klabu hiyo kujitokeza kwa wingi zaidi katika mkutano huo muhimu kwa maandeleo ya klabu.



Msikilize `Live` Asha Muhaji wakati akihojiwa na mtandao huu jioni hii


Bofya hapa chini


0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video