Mechi
 ya kwanza ya nusu fainali ya michuano ya mwaka huu ya Kombe la Chalenji
 kati ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) na wenyeji Kenya (Harambee 
Stars) itapigwa Uwanja wa Machakos.
Kwa 
mujibu wa ofisa wa CECAFA, Amir Hassan mechi hiyo itachezwa Uwanja wa 
Machakos ulioko takribani kilometa 64 kutoka jijini Nairobi. Mechi hiyo 
itachezwa Jumanne (Desemba 10 mwaka huu) kuanzia saa 10 kamili jioni na 
itaoneshwa moja kwa moja  na kituo cha televisheni cha SuperSport 
kupitia chaneli ya SS9.
Kilimanjaro
 Stars imetinga hatua hiyo baada ya kuivua ubingwa Uganda (The Cranes) 
kwa mikwaju 3-2 ya penalti katika mechi ya robo fainali ya michuano hiyo
 iliyochezwa jana Uwanja wa Aga Khan katika Jiji la Mombasa.
Hadi 
dakika 90 za kawaida zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana mabao 
2-2. Mabao ya Kilimanjaro Stars yalifungwa na Mrisho Ngasa wakati katika
 mikwaju ya penalti walofumania nyavu ni Amri Kiemba, Athuman Idd na 
nahodha Kelvin Yondani.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)


0 comments:
Post a Comment