Monday, November 4, 2013

masajuundp
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali , George Masaju

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
 Serikali imeandaa mafunzo   ya majadiliano  ya mikataba  kwa   wataalamu   mbalimbali  ili kuwapa mbinu za  kuendesha  mikataba  ya kibiashara  inayohusu rasilimali  za nchi  kwa manufaa ya Watanzania.
 Kauli  hiyo imetolewa leo na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali , George  Masaju  wakati wa ufunguzi wa semina ya wiki moja  kuhusu  majadiliano ya mikataba   inayoendelea kwenye hoteli ya  Bahari Beach jijini Dares Salaam  iliyohusisha  maaofisa waandamizi wa Serikali  kutoka  maeneo  tofauti.
 “Nchi yetu hivi  sasa iko katika mikakati ya kutumia rasilimali  zilizopo kwa ajili ya maendeleo  ya Watanzania  kupitia Sheria ya Ubia ya Pamoja  kutoka sekta  binafsi(PPP) kwa kuwahusisha wawekezaji wa ndani na nje.
“ Mafunzo haya yawatawasaidia  kufanya kazi kwa ufanisi na kuweza  kukabiliana na kampuni  kubwa zenye uwezo wa kifedha,katika  mikataba  inayohusu  madini , mafuta gesi ,nishati, Kilimo kwanza  ili kuhakikisha tunapata faida,” alisema  Masaju.
Aliongeza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa Dira ya Maendeleo ya Taifa ifikapo mwaka 2025 Tanzania iwe nchi nyenye kipato cha kati. Hivyo nchi yetu bado inawahitaji wataalamu kwenye maeneo  hayo.
 
Alisema  mafunzo hayo yamehusisha mawakili tisa  kutoka katika ofisi hiyo  na wengine toka taasisi mbalimbali za umma .
 Aliwataka  washiriki wasemina  hiyo kutumia mafunzo hayo kwa ajili ya kubadilishana mawazo na kupeana uzoefu juu  ya suala hilo.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Taasisi ya Uongozi .

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video