Thursday, November 28, 2013

Diamond1 
Na Ashura Mohamed – Arusha
Msanii wa muziki wa Kizazi kipya Diamond Platnum anatarajia kupagawisha  mashabiki wake wa  jiji la Arusha  siku ya Jumamosi  ya  tarehe 30 katika viwanja vya Hoteli ya Mount Meru.
Akizungumza na waandishi wa habari muandaji wa shoo hiyo Faustine Mwandago ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwandago Investment alisema kuwa maandalizi yote ya awali ya shoo hiyo iliyopewa  jina  la  Usiku wa  Wasafi na itakata kiu ya mashabiki wa Diamond waliopo jijini hapa.
Alisema kuwa msanii huyo ambaye ni maarufu ambaye  anasifika kwa kutoa burudani ya nguvu pindi anapokuwa jukwaani yupo tayari  kutoa burudani ya aina yake na anatarajiwa kuwasili jijini hapa siku ya siku ya Ijumaa.
Aidha mwandago alisema kuwa shoo hiyo ni ya aina yake kwa kuwa Diamond hajawahi kuja kwa ajili ya kufanya burudani kwa muda mrefu hivyo basi shoo hiyo ni kwa ajili ya kutoa burudani kwa mashabiki wake.
“Tumezoea kumuona Diamond kwenye shoo za Mamiss kama Miss Arusha na nyinginezo lakini kwa sasa hivi anakuja kwa ajili ya kutoa burudani tu kwa mashabiki wake hivyo naamini kuwa shoo hiyo itakata kiu kwa watakaohudhuria.”alisema mwandago
Akifafanua kuhusu shoo hiyo Mwandago alisema kuwa vazi litakalovaliwa kwa siku hiyo ni jeupe kwa kuwa ni Usiku wa Wasafi.
“Unapozungumzia vazi jeupe maana yake ni lazima uwe msafi kwa kuwa halipendi bugudha  hivyo tumeona dress code iwe nyeupe ili tuwakilishe vyema jina la Shoo la Usiku wa Wasafi”alisema Mwandago
Mbali na burudani kutoka kwa msanii huyo wasanii wanaochipukia kama Marry,Kandisi,Roggerz na madansasa wa boda boda waliopo chini ya Mwandago Investment watapamba shoo hiyo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video