Friday, November 1, 2013

url
ohn William `Del Piero`, kocha Njombe Mji fc
J
KUFUATIA soka la Tanzania kuendelea kukumbwa na vurugu za mashabiki hasa pale timu zao zinapofanya vibaya, wadau wa soka waendelea kukiponda kizazi cha wapenzi wa soka wa miaka ya leo kwa kukosa uvumilivu na kushindwa kuelewa zana halisi ya michezo.
Kocha wa timu ya soka ya Njombe mji inayoshiriki ligi ya mkoa wa Njombe na mjumbe wa kamati ya ufundi ya klabu ya Simba Sc na mdau wa siku nyingi wa soka la Tanzania, John W     iliam maarufu kwa jina la `Del Piero` amelaani vurugu zinazofanywa na mashabiki wa soka hapa nchini.
Piero amesema hayo baada ya kushuhudiwa vurugu kubwa zilizofanywa na mashabiki wa klabu ya Njombe Stand FC wakati wa mchezo wa ligi ya mkoa wa Njombe mara baada ya kufungwa mabao 3-0 mpaka dakika ya 60, hivyo kundi kundi kubwa la mashabiki lilivamia uwanja.
“Jana (juzi) tulikuwa na mchezo dhidi ya Njombe Stand fc, ni mechi ya watani wa jadi, mpaka dakika 45 timu hizi zilikuwa suluhu, kipindi cha pili timu yangu ilipata mabao matatu ya haraka na ndipo mashabiki walipoanza vurugu kwa kutoridhishwa na matokeo. Tabia hii si ya kimichezo kabisa”. Alisema Piero.
Piero alisema vurugu hizo sio tu kwa ngazi ya chini, bali hata ligi kuu kumekuwepo na mwendelezo wa matukio kama hayo ya utovu wa nidhamu katika soka.
Ametolea mfano pale mashabiki wa Yanga walipofanya vurugu na kupasua vioo vya gari la Coastal Union baada ya sare ya 1-1 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam,  pia mashabiki wa Simba jana walifanya vurugu na kung`oa baadhi ya viti vya uwanja wa Taifa kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Kagera Sugar kwenye uwanja huo huo wa Taifa.
vurugu10
Mashabiki wanaodhaniwa kuwa wa Simba sc jana walinyofoa viti vya kutosha uwanja wa Taifa baada ya sare ya 1-1 na Kagera Sugar. (Picha na Bin Zubeiry)

“Mashabiki wa timu kubwa za Simba na Yanga wanaona kuwa wao ndio wenye haki ya kushinda, kumbe siku hizi mpira hauko hivyo, unaweza kuwa na uwezo mkubwa na wachezaji wakubwa, lakini ukafungwa. kila timu inaingia uwanjani kushindana, hivyo mashabiki wawe na moyo wa kukubali matokeo”. Alisema Piero.
Pia Piero amegusia vurugu zilizotokea mkoani Mbeya ambapo Yanga walifanyiwa mchezo mchafu na mashabiki wa Mbeya City kwa kupasuliwa kioo cha mbele upande wa dereva wa  basi lao , lakini pia wiki hii wamewafanyia Tanzania Prisons vurugu hizo nje ya uwanja wakati timu hiyo inarudi kambini.
vurugu
Je, kuna sababu yoyote ya kufikia huku katika soka?, lazima watu wabadilike. (Picha na Bin Zubeiry)

“Tatizo la mashabiki wa soka wa Tanzania wanakwenda uwanjani na matokeo yao na inapokuwa kinyume wanafanya vurugu nje ya uwanja, watu hawa wapewe semina na vyombo vya usalama vitumie mamlaka yao kuwadhibiti watu hawa wanaochafua taswira ya soka la Tanzania”.
“Binafsi namuomba Rais mpya wa TFF, Jamal Malinzi na kamati zake kulichukulia uzito suala la vurugu kwani ipo siku kutatokea maafa makubwa zaidi kama ilivyowahi kutoka kwa nchi za wenzetu mfano Misri, Senegal na kwingineko”. Alisema Piero.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video