Thursday, October 31, 2013


MASHABIKISIMBA
Mashabiki wana mambo: Hawataki kufungwa hata kidogo
Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
WEKUNDU wa Msimbazi Simba SC wamelazimishwa sare ya bao 1-1 na wana `Nkulukumbi` Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara jioni hii uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Simba ndio walikuwa wa kwanza kuandika bao kupitia kwa nyota wake Amisi Tambwe, lakini dakika za lala salama, Kagera Sugar walipata penati iliyofungwa kwa ufundi na mkongwe na beki wa zamani wa Simba, Salum Kanon.
Hata hivyo hali ya uwanja iligeuka kuwa shari baada ya mashabiki wanaodhaniwa kuwa wa Simba kuanza kufanya vurugu na kung`oa viti vya uwanja wa Taifa hali iliyowalazimu polisi kuwatawanya kwa mabomu ya machozi.
Hali hii ilitokea baada ya kusawazishwa kwa bao hilo, kwani inaonekana mashabiki wa Simba walishajenga imani kuwa wameshinda mchezo huo na kusahau kuwa soka linahesabika kwa dakika 90.
Shuhuda wa MATUKIO DUNIANI uwanjani hapo ambaye ni mwandishi wa habari za michezo Mlimani TV na redio Mlimani ya Chuo kikuu cha Dar es salaam, Bwana. Fadhili Swala amesema baada ya kutolewa kwa penati hiyo, mashabiki wa Simba walionekana kutoridhishwa na kuanza kulaumu.
“Baada ya Kanon kufunga penati hiyo, mashabiki walionekana kujawa na jaziba na ndipo walianza kung`oa viti uwanja wa Taifa, lakini kwa sasa hali ni shwari baada ya polisi kutumia nguvu kuwaamuru kuondoka na kila mtu amekubali matokeo na kuamua kurejea nyumbani kwake kuendelea na majukumu mengine. Alisema Swala.
Pia alisema baada ya kipenga cha mwisho, kocha msaidizi wa Simba Sc, Jamhuri Kiwhelo `Julio` alionekana kumlaumu mwamuzi wa akiba kuwa walipunjwa muda.
Swala aliongeza kuwa mashabiki wengi waliohojiana na mtandao huu pale uwanjani wameonesha kukerwa na tabia hii ya utovu wa nidhamu kwani mpira una matokeo ya aina tatu, kushinda, kushindwa na kutoa sare kama ilivyotokea kwa Simba, hivyo hakuna haja ya kufanya vurugu.
Lakini inaonekana jaziba hii imetokana na matokeo ya mechi iliyopita ambapo Simba sc walilala dhidi ya Azam fc huku watani wao wa jadi wakishinda dhidi ya Mgambo Shooting mabao 3-0 na kukaa nafasi ya tatu katika msimamo.
Kwa kawaida matokeo ya timu za Simba na Yanga huwa yanaathiriana sana kwa mashabiki kwani mmoja akishinda anataka na yeye ashinde kwa vyovyote vile, kumbe hesabu za mpira hazipo hivyo.
Kutokukubali matokeo katika soka huwa kunaleta migongano na vurugu kama hizo uwanjani, hivyo lazima mashabiki wa soka wajifunze kuwa watulivu na kukubaliana na matokeo kwani haijaandikwa kuwa lazima Simba au Yanga ishinde katika mchezo, kila timu ina haki ya kushinda.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video