Thursday, October 31, 2013

mwl. kakore
Salamu za shukrani
Familia ya Kakore ya Dar es Salaam, tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa watu mbalimbali waliofanikisha shughuli nzima za mazishi ya ndugu yetu mpendwa, Mwalimu Jasper Rashid Kakore (71), aliyefariki ghafla asubuhi ya Jumapili, Oktoba 20 na kuzikwa Jumatano Oktoba 23 mwaka 2013.
Shukrani ziwafikie wafanyakazi wote wa Kampuni ya Gapco Tanzania, Kika Contraction, New Habari 2006 Ltd, Wizara ya Fedha (Hazina) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (Ukaguzi Kanda ya Mashariki), Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Pande, Wachungaji, Wainjilisti na watumishi wa K.K.K.T Usharika wa Mramba.
Pia wanachama wa Umoja wa Wanamtaa wa Tuna wa Dar es Salaam, Wanachama wa Umoja wa Wanakijiji wa Chome wa Dar es Salaam, Wafanyakazi wote wa Hospitali za Gonja, Apolo na Hospitali ya Wilaya ya Same, wafanyakazi na wanafunzi wa Shule za Sekondari Same na Dindimo.
Kadhalika tunapenda kuwashukuru Wanakijiji wa Gonja na Wanamtaa wa Vuje pia mitandao mbalimbali ya kijamii (Blogs) ndugu, jamaa na marafiki.
Tunaelewa kuwa watu ni wengi waliojitoa kwa ajili yetu hivyo kwa yeyote ambaye kwa namna moja ama nyingine hatukuweza kumtaja tunaomba radhi ila tunathamini sana kile ulichokitoa kwa ajili yetu.
Kama familia hatuna la kuwalipa ila Mungu aliyewapa moyo wa kujitoa ndiye atakayewarudishia mali na kila mlichotoa kwa ajili yetu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video