Friday, September 13, 2013


Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
KOCHA Arsene Wenger amesema hatima yake kuinoa Asernal akiwa kocha mkuu itaamuliwa na kufanikiwa au kushindwa kupata mafanikio katika kikosi chake anachokijenga kwa sasa baada ya kumsajili na Mesut Ozil na kuvunja rekodi ya klabu yake.
Mkataba wa Wenger unamalizika mwezi juni mwakani amesema aliamua kumsajili kiungo huyo Mjerumani kwa ada ya pauni milioni 42.5 akiwa na lengo la klabu yake kuwekeza zaidi na kupata mafanikio makubwa.
Alipoulizwa jana kama amefungua mazungumzo kuhusu mkataba mpya, kocha huyo mwenye miaka 63 alisema: “Hatuna haraka. Tuko mwezi wa tisa na mkataba unamalizika juni mwakani. Kuna muda mrefu kuzungumza hilo. Hukuna haja ya kupanga”.
Uncertain future: Arsene Wenger lined up alongside new signing Mesut Ozil at Thursday's press conference 
Hatima ya baadaye haijulikani: Arsene Wenger akiwa na nyota wake mpya Mesut Ozil hapo jana katka mkutano na waandishi wa habari

Colney training: Arsene Wenger, Mesut Ozil, Per Mertesacker and assistant manager Steve Bould 
Mazoezini Colney: Arsene Wenger, Mesut Ozil, Per Mertesacker na kocha msaidizi Steve Bould
Trophyless: Arsenal's last silverware was the 2005 FA Cup won at the Millennium Stadium 
Ukame wa makombe: Arsenal kwa mara ya mwisho walinyanyua kombe la FA 2005 katika dimba la Millennium
“Nimekuwa nikisema mara nyingi kuwa nataka kufanya vizuri na timu hii na mwishoni nitakaa chini na kutafakari ni kwa namna gani nimefanikiwa. Hiyo itatosha kwangu kuamua kama nitabaki au la”. Alisema Wenger.
“Moja kati ya mambo makubwa ya kocha ni kuona namna gani amefanikiwa akiwa na timu”
Ozil anaamni anaweza kumaliza ukame wa miaka nane kwa Asernal bila kutwaa kikombe na anaamini kikosi chake kinaweza kushinda msimu huu wa ligi kuu soka nchini England.
Baada ya kuondoka Real Madrid, Ozil amesisitiza kuwa ujio wake London kaskazini sio kushuka kwake.
“Sijakata tamaa. Nipo Arsenal sasa, ni moja kati ya klabu kubwa duniani”
“Kiukweli nilikuwa na wakati mzuri Madrid. Nimewapoteza rafiki zangu na muda mzuri pale. Sasa nipo ligi ngumu zaidi duniani na natakiwa kuwahakikishia kuwa nitaendelea kukua zaidi. Na ndio maana nipo katika klabu sahihi”. Alisema Ozil.
Top dog: Arsene Wenger broke Arsenal's transfer record to bring Mesut Ozil from Real Madrid 
Jembe jipya: Arsene Wenger alivunja benki ya Arsenal na rekodi ya klabu katika usajili wa Mesut Ozil kutoka Real Madrid

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video