Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney hatimaye amekubali kubaki na kukubali ukweli kuwa hawezi kuruhusiwa kuihama klabu yake na kujiunga na Chelsea.
Japokuwa ameonesha nia ya kutaka kufanya kazi na Jose Mourinho, Rooney ameamua kutulia ili aimarike zaidi baada ya kukosa mechi zote za maandalizi ya msimu mpya kutokana na kukumbwa na majeruhi.
Nyota huyo kwa mara ya kwanza alicheza jana chini ya kocha David Moyes katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu dhidi ya Swensea City ambapo United walishinda kwa mabao 4-1, huku akitoa pasi mbili zilizozaa mabao, lakini hakujiunga na wenzake kushangilia mabao hayo.
Mbali kabisa: Wayne Rooney (wa pili kushoto) alionekana kutoshangilia bao la tatu na wenzake licha ya kusababisha yeye
Hana mpango: Rooney (wa nane kulia) akipiga stori na mwamuzi wa mchezo wa jana Phil Dowd wakati wachezaji wenzake wa United wakijumuika na Danny Welbeck kushangilia bao la nne
Tulia kijana wangu, shida ya nini?: Rooney atabakia kuwa mchezaji wa Manchester United msimu huu
Akipata maelekezo, ingia pale nenda kapike mambo, sawa?: Rooney aliingia dakika ya 61 akichukua nafasi ya kocha mchezaji Ryan Giggs, na kusababisha magoli mawili 
0 comments:
Post a Comment