Monday, July 15, 2013


Na Baraka Mpenja

Siku chache baada ya uongozi wa wekundu wa Msimbazi Simba kumrejesha kundini kiungo wake mahiri mwenye uwezo mkubwa wa kupaka rangi mpira, Ramadhan Suleiman Chombo “Redondo” amefunguka na kuweka wazi kuwa nafasi hiyo ni muhimu kwake kwani bado anathimini mchezo wa soka kuwa ni ajira yake rasmi inayomfanya ale, avae na kufanya mambo mengi yahusuyo  maisha maisha yake.


Redondo aliyesimamishwa pamoja na wenzake , Washambuliaji, Ferlix Sunzu na Abdallah Juma, mabeki Juma Nyoso, Paul Ngalema, na viungo Haruna Moshi “Boban”,  na Mwinyi Kazimoto Mwitula, amerudishwa katika kikosi cha Abdallah Kibadeni, pamoja naye  Kazimoto aliyerudishwa  muda mrefu, wakati Sunzu alimaliza mkataba wake na wengine wametemwa moja kwa moja.


Akizungumza na MATUKIO DUNIANI, Redondo amesema kusimamishwa kwake kulimuuma sana kwani alikuwa mgonjwa baada ya kutoka Angola kucheza mechi ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Libolo, mechi ambayo Simba walifungwa mabao 4-0.


“Unajua nilisimamishwaje ndugu yangu?, tulipotoka Angola kucheza na Libolo na kurejea Dar es salaam, mimi ni Mwinyi Kazimoto tulipata maleria, baada ya kupona na kwenda mazoezini, tukashangaa kocha anasema hatutaki mazoezini na ndipo tuliposimamisha. Na wengine waliofuta mbele yetu mfano Abdallah Juma wote walisimamishwa, niliumia sana, lakini sikuwa na jinsi”. Alisema Redondo.

 Redondo  aliongeza kuwa kurejea kwake Simba ni muhimu sana na atafanya vizuri na kuwafurahisha mashabiki wa Simba ambao kwa sasa wana uchu mkubwa wa kuona timu yao inafanya vizuri msimu ujao.
“Nitacheza kwa kujituma zaidi, nakumbuka siku moja tuliwahi kuzungumza na wewe nikiwa Azam fc kuwa baada ya Kagame nitarudi timu ya taifa, na ikatokea hivyo, nadhani unakumbuka, daima mimi najua mpira ni kazi yangu, nitajituma zaidi kwa kuisaidia timu yangu”. Alisema Redondo.

Pia alisisitiza kuwa ifike wakati wachezaji wanatakiwa kuthaminiwa sana kama nchini za wenzetu, hata zawadi wanazopewa baada ya kufanya vizuri ni muhimu zikathaminiwa zaidi ili kuamsha ari ya mpira wa Tanzania.


“Wakati nikiwa Azam, rafiki yangu Ngassa alipewa kiatu dhahabu cha mfungaji bora, lakini ni kama mbao Fulani, kilichofanyika ni kupuliziwa rangi ya dhahabu tu, nilimuuliza utaweka nyumbani kweli hii mwanangu? Akaniambia hii kitu nitampa tu mwanangu achezee. Afrika kusini wenzetu wameendelea, na sisi tuige mfano wao, tuthamini vipaji”. Alisisitiza Redondo.

Redondo alisema kuwa kuna wachezaji wengi wameacha mpira bila sababu, na kitu kikubwa kinachowasababisha ni magumashi na fitina za viongozi wa soka ambao mara zote hawathamini vipaji vya soka.

“Kwa mfano leo hii Shaban Kisiga wanamuita mzee, lakini yule jamaa ni bonge la mchezaji, kushindwa kuthamini kipaji chake ndio sababu ya kumuona kama hana maana. Sio yeye tu, wapo wengi zaidi ya yeye, hata wewe unawajua ndugu yangu”. Alisema Redondo.
Wakati huo huo rafiki yake Redondo ambaye ni shabiki wa kutupwa wa klabu ya Yanga ya Dar es salaam Bwana Yahya Uyagwa alifurahishwa na kitendo cha rafiki yake kurudi Simba ili waandeleze utani wao.

“Mimi bwana nampenda sana huyu jamaa, mimi ni shabiki wa Yanga, lakni Redondo ni mshikaji wangu wa kufu mtu, nimefurahi sana kurejea Simba, nadhani atafanya vizuri kwani anajituma sana”. Alisema Uyagwa.

Uyagwa aliongeza kuwa mara nyingi Yanga ikiwafunga Simba anamcheka sana Redondo, lakini yanaisha uwanjani na baada ya hapo wanafikiria maisha mengine  nje ya mpira, ila amemsifu rafiki yake kwa kuwa mvumilivu na kujua kazi yake vizuri.



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video