Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mashetani wekundu, Manchester United, rasmi wamefungua njia kwa mshambuliaji wao Wayne Mark Rooney baada ya kusema hawana mpango wa kukaa chini na nyota huyo kuhusu kusaini mkataba mpya wa kuichezea klabu hiyo na wanachohitaji kwa sasa ni kumuangalia uwezo wake uwanjani kabla ya kukaa mezani kujadili hatima yake Old Trafford.
Mkurugenzi mkuu wa United Ed Woodward alithibitsha hilo jana wakati klabu yao ikishuka dimbani katika mchezo wa kwanza tangu waanze ziara yao nchini Thailand ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu ambapo alisema kipaumbele kwa sasa nikuangalia dili la uhamisho kama litalipa na sio kuweka nguvu kubwa ya kukaa na Rooney kujadili hatima yake.
Roonye bado amebakiza miaka miwili katika mkataba wake ambao anakunja kitita cha pauni laki mbili na nusu kwa wiki.
Kwasasa mshambuliaji huyo amerudi nchini England baada ya kupata majeraha ya nyama za paja,huku akihusishwa na mpango wa kutimkia konako Chelsea au kwa matajiri wa Ufaransa , Paris St-Germain, lakini imeshaelezwa na United kuwa nyota huyo baba wa watoto wawili hatauzwa majira haya ya kiangazi.
Woodward alisema: ‘Hakuna majadiliano yoyote yaliyofanyika juu ya kuongezwa kwa mkataba. Sijakaa na mchezaji yeyote kujadili kuongeza mkataba wake na hakuna chochote kwenye kitabu changu cha kumbukumbu”
‘Tunaweza kuongopa kuvunjika kwa mkataba na Mchezaji? kiukweli hapana”.
Rooney hakuwepo katika kikosi cha jana cha David Moyes ambapo aliiongoza United katika mechi ya kwanza dhidi ya Singha All-Stars mjini Bangkok na kupoteza kwa kufungwa bao 1-0.
Kauli hii ya kibosile huyo wa United imeongeza nguvu kwa kocha wa Chelsea, Jose Mourinho ambaye alisema yupo tayari kumwaga kitita cha pauni milioni 60 ili kumnasa Rooney, lakini naye Laurent Blanc wa PSG amekodoa macho yake kwa nyota huyo.
Hakuna mipango: Wayne Rooney, akiwalsili nyumbani Manchester, hataweza kujadili mkataba mpya na United
Mgogoro mkubwa: Bosi wa Chelsea , Jose Mourinho alitangaza nia ya kumhitaji Rooney, lakini David Moyes (chini) amesema nyota huyo hauzwi
Changamoto Mpya: Jana amepata wakati mgumu katika mechi yake ya kwanza kuiongoza United, lakini hata kibabu Sir Alex Ferguson enzi zake alianza kwa kufungwa mechi ya kwanza
Chali: Moyes akitazama mechi yake ya kwanza ambayo alipoteza dhidi ya Singha All-Stars iliyopigwa Bangkok
Kinda la ukweli: Adnan Januzaj akimkimbiza mchezaji wa Singha All-Stars kwenye mechi yao ya kwanza ziarani mashariki ya mbali
Fundi: Tom Cleverley akijaribu kumiliki gozi la ng`ombe, lakini hii haikusaidia kuzuia United kufungwa jana
Kocha mpya wa PSG, na beki wa zamani wa United, Laurent Blanc, pia anamtaka Rooney
Mshindi: Rooney aliisaidia United kutwaa ubingwa msimu uliopita, lakini anahusishwa na kutaka kuihama klabu hiyo majira haya ya kiangazi
Akishangilia: Rooney amekuwa mchezaji muhimu sana tangu kutua Old Trafford mwaka 2004, lakini kwa sasa anataka kuihama klabu hiyo 
0 comments:
Post a Comment