Monday, July 1, 2013


Uganda-Jackson-Mayanja-300
Na Baraka Mpenja 
Wakata miwa wa Kagera Sugar wenye makazi yao Kaitaba kanda ya ziwa mkoani Kagera wamesema kocha wao mpya,  Mganda Jackson Mayanja ambaye alikuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Uganda ni bora zaidi ya Kibadeni kwani yeye ndiye aliyesuka kikosi ambacho kocha huyo aliyetimkia kwa wekundu wa msimbazi Simba alikiongoza msimu uliopita.
Afisa habari wa klabu hiyo, Hussein Mohamed amezungumza na MATUKIO DUNIANI kwa njia ya simu kutoka Kaitaba na kubainisha kuwa klabu yao inatambua sana mchango wa mwalimu Kibadeni, lakini aliwakuta wachezaji wameshaiva baada ya kunolewa na kocha Mayanja, na sasa amerejea mwenye timu, hivyo wana imani kubwa sana msimu ujao watafanya makubwa zaidi.
“Kwa sasa tunaendelea na usajili wetu, kesho tunamalizana na mchezaji kutoka Africa Lyon, Adam Kingwande ambaye tunaamini atatuongezea kasi zaidi katika safu yetu ya ushambuliaji”. Alisema Mohamed.
Mohamed alisema mazungumzo na Kingwande yamemalizika, huku akisema wanatambua kuwa wana tatizo katika safu ya ushambuliaji, na suluhusho ni nyota huyo mwenye makali ya kutosha.
“Timu yetu haijabadilika sana, tumepoteza wachezaji wawili, kiungo Juma Nadi aliyetimkia Ruvu Shooting na Andrew Ntalla aliyenaswa na Simba, hivyo hatuna  kazi kubwa sana ya kuziba nafasi”. Alisema Mohamed.
Afisa habari huyo alisema timu hiyo itaanza mazoezi rasmi julai 10 mwaka huu katika dimba la Kaitaba na kocha wao Mayanja anatarajiwa kuwasili kati ya julai 8 tayari kwa kuanza program yake ya mazoezi.
Mohamed alisisitiza kuwa msimu ujao wanajiandaa kuhakikisha wanashika nafasi nzuri zaidi na kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya kimataifa.
Msimu uliopita Kagera walimaliza ligi kuu wakiwa nafasi ya nne, huku Simba, Azam fc na Yanga wakiwa juu yao.
Mafaniko hayo yalifikiwa chini ya kocha Abdallah Kibadeni “King Mputa” na sasa kocha huyo mzawa amepata shavu kwa wekundu wa msimbazi ambaye ndiye kocha mkuu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video