Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha Arsene Wenger amepata pigo baada ya beki kisiki wa klabu hiyo, Laurent Koscielny kugongana na mlinda mlango Wojciech Szczesny na kuumia, hivyo atakaa nje ya uwanja katika mchezo wa kirafiki wa kesho mjini Nagoya.
Beki huyo alitoka katika mazoezi mwishoni na kuonekana mwenye maumivu ya kifundo cha mguu.
Timu ya matibabu wa Asernal walimchunguza tatizo lake kabla ya kuondolewa katika dimba la Mizuno Rugby kwa ajili ya matibabu zaidi.
Inafahamika kuwa nyota huyo alikuwa na maumivu tangu wawasili ijumaa nchini Japan.
Hata hivyo Lukasz Fabianski au Damien Martinez watachukua nafasi ya Szczesny katika mechi dhidi ya Nagoya Grampus.
Taarifa za kuumia kwa Koscielny zinamaanisha Wenger atamkosa moja ya mabeki wake wenye uzoefu, Per Mertesacker; katika ziara yake ya mashariki ya mbali, ingawa atamtumia zaidi kinda wake Ignasi Miquel
Wenger tayari hanaye Thomas Vermaelen, ambaye tupo nje ya uwanja kwa miezi mitatu.
Laurent Koscielny alikuwa katika morali kubwa katika mazoezi ya leo kabla ya kuumia
Mtu maarufu: Theo Walcott akisaini vitabu vya kumbukumbu vya mashabiki mjini Nagoya

Anatoa maelekezo: Arsene Wenger akizungumza na mashabiki wakati wa mazoezi
Walinzi wakiwadhibiti mashabiki waliokuwa wanasubiri kuwasili kwa nyota wao kutoka kaskazini mwa Londo
Mwaga wino hapa jamaa: Bacary Sagna akipita kwa taabu katika mkusanyiko wa mashabiki wa Arsenal wakati akiingia uwanja wa mazoezi
Vijana wa Arsenal wakipasha moto misuli nchini Japan 
Furaha kubwa kuwepo hapa: Nyota wa England, Alex Oxlade-Chamberlain na Theo Walcott wakipozi katika picha wakati wa mazoezi
Tabasamu: Lukas Podolski akiwa katika basi na kukaa pozi la tabasamu na kupigwa picha
Podolski aligeuka mpiga picha wakati wa mazoezi nchini Japan
Akitazama kwa umakini: Per Mertesacker wakati wa mazoezi nchini Japan
Majeruhi ya Koscielny yatamfanya kocha Wenger aongeze haraka kumsajili beki wa muda mrefu ambaye amuwania kutoka Swansea City, Ashley, Williams.

0 comments:
Post a Comment