Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
 MSHAMBULIAJI
 Mario Balotelli alifunga bao la ushindi kwa Italia, baada ya Andrea 
Pirlo kutangulia kufunga bao la kuongoza kwa mpira wa adhabu akiichezea 
nchi yake mechi ya 100 katika mchezo wa Kundi A Kombe la Mabara.
 Balotelli
 alipokea nzuri ya Emanuele Giaccherini zikiwa zimesalia dakika 12 na 
akapasua katikati ya mabeki wawili kabla ya kufunga kwenye Uwanja wa 
Maracana.
 Mshambuliaji
 wa Manchester United, Javier ‘Chicharito’ Hernandez alifunga kwa 
penalti dakika ya 34 kuipa Mexico bao la kusawazisha baada ya Andrea 
Barzagli kumuangusha kiungo wa zamani wa Tottenham, Giovani Dos Santos 
kwenye boksi.
 Hernandez anaelekea kuipiku rekodi ya mabao mengi Mexico, 42 yaliyofungwa na gwiji wa zamani wa nchi hiyo, Jared Borgetti.
 Mchezaji
 bora wa mechi alikuwa Pirlo aliyefunga bao la kwanza dakika ya 27 
akimtungua kwa mpira wa adhabu kipa wa Mexico, Jose de Jesus Corona.
 Kikosi
 cha Mexico kilikuwa: Corona, Rodriguez, Salcido, Flores, Moreno, 
Torrado, Aquino/Mier dk53, Zavala/Jimenez dk85, Guardado, Giovani na 
Hernandez.
 Italia: Buffon,
 Chiellini, De Sciglio, Abate, Barzagli, Marchisio/Cerci 68, De Rossi, 
Montolivo, Pirlo, Giaccherini/Aquilani dk88 na Balotelli/Gilardino dk85.

 
Balotelli akiandika bao kimiani


 Mpenzi wa Balotelli, Fanny Neguesha akifurahia mechi kwa kupiga picha
 
 Javier ‘Chicharito’ Hernandez aliifungia kwa penalti Mexico





0 comments:
Post a Comment