Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha
 machachari na mwenye maneno mengi Mario Jose Dos Santos Mourinho 
anamkodolea macho mchezaji  Kiungo Luka Modric wa Real Madrid ili 
aondoke naye kuelekea zake klabu ya Chelsea.
Mourinho
 alithibitisha wiki iliyopita kuwa anaondoka Real na anataka mchezaji 
huyo wa zamani wa klabu ya Tottenham kuambatana naye katika safari yake 
hiyo ya kuelekea darajani.
Kiungo huyo mwenye uwezo mkubwa ataigharimu Chelsea pauni milioni 30 ili kutia maguu yake darajani.
Habari
 za ndani kutoka klabu ya Chelsea zinaeleza kuwa “Mourinho yuko makini 
kufuatilia suala la Modric na lazima atue nae darajani, tunajua ni kazi 
ngumu sana lakini tunamuamini sana kocha wetu”.
Modric
 mwenye miaka 27 hajafanya kubwa sana nchini Hispania, lakini Mourinho 
bado amejenga imani kubwa sana licha ya kucheza mechi 31 tu katika msimu
 wa ligi kuu ya La Liga.
WANARUDI : Modric na Mourinho wote wanatarajiwa kurudi ligi kuu soka nchini Uingereza League 
 
Mourinho yuko makini kumuwinda Modric ili asepe naye kuelekea Chelsea
 
Modric amekuwa na msimu mgumu sana Real Madrid lakini Mourinho bado ana imani kubwa sana na nyota huyo raia wa Croatia 
 
Chelsea  wana Historia ya kumhitaji Modric na mnamo mwaka 2011 walituma ofa mbili lakini Spurs walizitupilia mbali
 
ANARUDI: Mashabiki wa Chelsea wameonesha nia ya kumtaka  Mourinho  darajani 

0 comments:
Post a Comment