WAREMBO wenye sifa za kushiriki shindano la Redds Miss Tanga, wametakiwa kujitokeza kushiriki shindano katika kuwania taji la Miss.
Akizungumza na Vyombo vya Habari 
Mkurugezi wa Kampuni ya datk Intertaimeint, Asha Kigundula alisema kwa 
maandalizi ya shindano hilo ndiyo yanaanza na kutaka warembo wajitokeza 
kushiriki.
Asha alisema fomu zitapatikana 
katika ofisi ya Mwananchi iliyopo bandari Tanga gorofa ya Nne, Five 
brathers kwa nassa makau iliyopo jijini humo, kwa Dar es Salaam 
zinapatikana katika ofisi za Jambo Leo zilizopo jingo la Hifadhi Hause 
Posta.
“Mazoezi kwa warembo yataanza 
ijumaa ya Mei 3 mwaka huu jijini Tanga, warembo hao watakuwa chini ya 
walimu wawili ikiwa ni pamoja na mshindi wa mwaka jana wa mkoa huo 
Teresia Kimolo”alisema Asha.
Alisema kwamba shindano la mwaka 
huu litaandika historia mpya ya urembo mkoani humo kwa kuwa Kampuni datk
 imejipanga, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wa jijini hapo kwa 
ujumla wakae mkao wa kupata raha.





0 comments:
Post a Comment