Mshambuliaji nguli wa JKT Ruvu Mussa Hassan Mgunya “Mgosi” (kulia) akifanya vitu vyake katika mechi dhidi ya Yanga 
 
 
 
Kikosi cha Prisons kinachotaraji kushuka ugani siku ya mei mosi dhidi ya JKT Ruvu
Na Baraka Mpenja
Wakichagizwa
 na ushindi wa 1-0 dhidi ya Africa Lyon wiki hii, maafande wa jeshi la 
kujenga taifa JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani wapo katika morali kubwa 
kujiandaa na mchezo wa mei mosi dhidi ya wanajeshi wenzao kutoka jijini 
Mbeya “Jiji la Kijani”, Wajelajela Tanzania Prisons uwanjwa wa Chamazi 
Mbande nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo Greyson Haule ameiambia MICHEZO BOMBA!
 kuwa mpaka sasa wachezaji wote wako salama, hakuna majeruhi yeyote na 
wana morali kubwa kutokana na kuwepo katika mikono salama ya kusalia 
ligi kuu Tanzania bara msimu huu.
“Sisi
 tuko makini sana, wachezaji wangu wote wako barabara, tunarekebisha 
makosa madogo madogo yaliyoonekana mechi iliyopita, nadhani kufikia siku
 ya mechi tutakuwa fiti kuwavaa Prisons”. Alisema Haule.
Haule
 aliongeza kuwa mechi hiyo itakuwa ngumu sana kutokana na timu hizo kuwa
 sambamba katika msimamo,  wote wakiwa na pointi 26 lakini Prisons wapo 
juu yao kufuatia wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Prisons yupo nafasi ya 9 wakati Ruvu wapo nafasi ya 10 katika msimamo.
Timu 
zote mbii zitaweza kusalia ligi kuu bara msimu huu kwani zina pointi 
nzuri na zinaweza kujichimbia zaidi endapo zitachanga kwa uzuri karata 
zao za mwishoni.
Wakati huo huo maafande wa Tanzania Prisons leo hii wapo njiani wakisafiri kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya mechi hiyo.
Katibu
 mkuu wa klabu hiyo Sadick Jumbe alisema wamefanya maandalizi ya kutosha
 na wameamua kufika siku mbili kabla ya mchezo ili wachezaji wapumzike 
kabla ya kipute hicho.
“Tuko
 vizuri, wachezaji wote wapo salama na wana morali kubwa sana kuibuka na
 ushindi, akina Elias Mguli, Sino Augostino, Henry Mwalugala, Lugano 
Mwangamba na wengine wengi wote wana morali kubwa kuwaadhibu JKT Ruvu 
mei mosi”. Alisema Jumbe akiwa njiani.






0 comments:
Post a Comment