Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Mikikimikiki
 ya ligi kuu Vodacom Tanzania bara inatarajia kuendelea jioni ya leo 
katika dimba la taifa ambapo waliokuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo, 
wekundu wa msimbazi Simba “Taifa kubwa” watawakaribisha wapiga kwata wa 
Polisi Morogoro katika dimba la taifa maeneo ya Chang`ombe jijini Dar es
 salaam.
Mchezo huo unatarajia kuwa mkali kutokana na umuhimu wa matokeo ya ushindi kwa timu nzote mbili.
Mnyama
 Simba ambaye tayari ameshapoteza ubingwa wake na kuwakabidhi watani 
zake wa jadi Dar Young Africans “Kwalalumpa Malysia” anahitaji ushindi 
kufa na kupona ili kupigania angalau nafasi ya pili na kulinda heshima 
yake.
Simba
 ambaye msimu huu mambo yamemwendea mrama anatarajia kutumia kikosi 
kilekile cha makinda wake ambao wanawajenga kwa ajili ya msimu ujao, pia
 kujiandaa kukumbana na Yanga mechi ya funga pazia ya ligi kuu msimu wa 
2012/2013 uwanja wa taifa mwezi mei mwaka huu.
Akiongea na MICHEZO BOMBA!
 Kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto” aliseama leo 
hii mchana wamekaa kikao na wachezaji wao ili kuwapa morali na kuwaeleza
 umuhimu wa kushinda katika mchezo wa leo.
“Ninavyokuambia
 hivi tupo katika kikao cha pamoja na wachezaji wetu, tunaelezana 
machache kabla ya kwenda uwanja wa taifa kuvaana na polisi Morogoro, 
maandalizi yetu ni mazuri na tuna imani ya kushinda”. Alisema Julio.
Julio
 aliongeza kuwa mashabiki na wanachama wa wekundu wa smimbazi Simba 
lazima watambue kuwa timu yao ipo wakati wa mpito, kinachotakiwa kwa wao
 ni kuwaunga mkono vijana wao ambao wanajengwa kuleta matunda msimu ujao
 wa ligi.
“Leo 
hii watu wanaiona Simba haina lolote, sisi tunasema hiki kikosi ambacho 
kinaandaliwa na benchi la ufundi kitakuwa moto wa kuotea mbali sana, na 
siku zote tunamshukuru Mungu kwa kutupa uzima na tuna matarajio makubwa 
sana na vijana wetu”. Alisema Julio.
Wakati
 Mnyama akijinasibu kushinda mchezo wa leo, nao Polisi Morogoro walisema
 maandalizi waliyoyafanya yanatosha kupata ushindi mbele ya Simba.
Afisa habari wa klabu hiyo, Clememce Banzo ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa endapo watapoteza mchezo wa leo watazidi kujichimbia kaburi wenyewe na kujizika ndani yake.
“Maji
 yameshafika shingoni, hakika hatuna hali mpaka sasa na tukifungwa na 
Simba, safari ya kutoa mkono wa bai bai kwa ligi kuu ya Tanzania bara 
itakuwa imeshafika”. Alisema Banzo akiwa amekata tamaa.
Banzo
 aliongeza kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo Rishard Adolf tayari amehawapa 
mazoezi mazuri na kuwapanga kisaikolojia wachezaji wake kupambana na 
simba leo hii.
Siku 
zote soka ni dakika tisini, aliyejipanga na kuwa na nidhamu ya mpira 
dimbani anaweza kupata ushindi, leo Simba ama Polisi yoyote anaweza 
kutwaa pointi tatu muhimu, dakika za mwamuzi zinasubiriwa.






0 comments:
Post a Comment