Mlinzi wa pembeni wa Tottenham
Hotspur Benoit Assou-Ekotto ametajwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon
(simba wasioshindika) ikiwa imepita miaka miwili bila kuwepo, ambacho kitacheza
mechi ya kirafiki iliyopo katika kalenda ya FIFA februari sita mwaka huu.
Benoit Assou-Ekotto |
Mlinzi huyo ametajwa katika kikosi
cha wachezaji 21 ambacho kinataraji kucheza na timu ya taifa ya Tanzania Taifa
stars februari 6 kwa mjibu wa taarifa kutoka shirikisho la Soka Cameroon.
Nyota huyo alikataa kuchezea timu ya
taifa ya Cameroon kwa madai ya mwenendo mbaya wa timu hiyo, lakini amekubali
baada ya kukutana na kocha Jean-Paul Akono.
Cameroon wataitumia mechi hiyo
kujiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la duni mnamo mwaka 2014
dhidi ya Timu ya taifa ya Togo mjini Yaounde machi 24 mwaka huu.
Katika kundi lake Cameroon ina
pointi 3 kwenye kundi lake la I
KIKOSI KIZIMA NI
Goalkeepers: Charles Itandje (Atromitos), Joslain Mayebi (Wrexham)
Defenders: Benoit Angbwa (FC Rostov), Benoit Assou-Ekotto (Tottenham
Hotspur), Henri Bedimo (Montpellier), Jean Armel Kana-Biyik (Stade Rennes),
Nicolas Nkoulou (Olympique Marseille), Romeo Allan Nyom (Granada), Pierre Wome
(Canon Yaounde)
Midfielders: Aminou Bouba, Charles Eloundou (both Coton Sport), Jean
Makoun (Stade Rennes), Joel Matip (Schalke 04), Landry Nguemo (Girondins
Bordeaux), Alex Song (Barcelona), Herve Tchami (Honved)
Forwards: Vincent Aboubakar (Valenciennes), Achille Emana (Al Wasl),
Samuel Eto'o (Anzhi Makhachkala), Fabrice Olinga (Malaga), Jean Paul Yontcha
(Olhanense).
0 comments:
Post a Comment