Wednesday, November 30, 2016

Wekundu wa Msimbazi Simba SC wamethibitisha kumsajili kipa mpya Mghana Daniel Agyei aliyekuwa akikipiha kunako klabu ya Medeama ya nchini humo.

Kipa huyo ameondoka kwenye klabu hiyo maarufu kwa jina la Mauves baada ya kucheza kwa kipindi kisichozidi msimu mmoja.

Kupitia akaunti ya Instagram Simba wamethibitisha hilo kwa kuweka picha yake yenye maelezo yanayosomeka: "Golikipa Daniel Agyei amewasili rasmi nchini tayari kujiunga na kikosi cha Simba.

Agyei ,24, alijiunga na Medeama SC katika raundi ya pili ya  msimu kwenye Ligi Kuu nchini humo maarufu kama Ghana Premier League  baada ya kurejea kutoka nchini Afrika Kusini alipokuwa akicheza kunako klabu ya Free State Stars.

Mapema mwezi huu Agyei aliandika kwenye moja ya akaunti zake za mitandao ya kijamii kuthibitisha kuondoka kwake klabuni hapo.

“Sidhani kama kuna maneno yatakayotosheleza kiasi cha huzuni ninayoisikia kutokana na kuwaaga wote hapa kwenye klabu yangu pendwa ya Medeama SC, " alindika kwenye akaunti yake ya Facebook.

“Ningependa kuwashukuru viongozi, benchi la ufundi, wachezaji wenzangu pamoja na mashabiki kwa sapoti yao kubwa waliyonionesha kwa kipindi kifupi nilichodumu klabuni hapa. Medeama itabaki kuwa klabu itakayodumu moyoni mwangu milele.”

A photo posted by Simba SC Tanzania (@simbasctanzania) on


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video