Tuesday, November 29, 2016

Habari za kusikitisha katika ulimwegu wa soka ni kwamba, klabu ya Chapecoense ya Brazil imepata ajali baada ya ndege iliyokuwa imebeba wachezaji pamoja na viongozi kuanguka kwenye mji wa Medellin, Colombia.

Chapecoense ilikuwa imefika hatua ya fainali ya Copa Sudamericana, ambayo ni sawa na Europa League kwa Ulaya na walikuwa wanaelekea Medellin kwa ajili ya kucheza mchezo wao wa fainali dhidi ya Atletico Nacional siku ya Jumatano.

Mechi hiyo tayari imeshaahirishwa huku shirikisho la soka la Amerika ya Kusini (South American Football Confederation) limethimitisha kuahirisha shughuli zote kuhusiana na mchezo huo hadi watakapotoa taarifa baadae.


BBC wameripoti kwamba, taarifa za ajali hiyo bado zinachanganya lakini inaripotiwa kuna watu ambao wapo hai.

Kwa upande wao Globo wameripoti kuwa, kulikuwa na abiria 72 pamoaja na wafanyakazi 9 wa ndege hiyo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video