![]() |
Juma Nkamia |
UMOJA wa timu za ligi daraja la kwanza Tanzania
bara (FDL) kesho jumamosi unatarajia kufanya mkutano mkubwa na wa kihistoria
jijini Dar es salaam kujadili changamoto mbalimbali za ligi hiyo na kutafuta
namna ya kuzitatua au kuzipunguza.
Msemaji wa umajo huo, Masau Bwire amesema mgeni
rasmi atakuwa naibu Waziri wa Wizara ya Habari, vijana, utamaduni na Michezo,
Juma Nkamia atayeambatana na wageni waalikwa akiwemo Rais wa TFF, Jamal Malinzi
na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa, Dioniz Malinzi.
“Lengo kuu la mkutano huu ni kujaribu kuangalia
changamoto zinazoikabili ligi daraja la kwanza na namna tunavyoweza kuzitatua
au kupunguza. Pia ni kuangalia namna serikali na mamlaka za kusimamia mpira
zinavyoweza kufanya ili kuboresha ligi daraja la kwanza” Amesema Masau Bwire na
kuongeza: “Si tu kuboresha ligi daraja la kwanza, tuna mengi ya kuzungumza
kuhusu soka la Tanzania. Ni mkutanao wa kihistora ambao wajumbe wa klabu zote
24 vinavyounda ligi daraja la kwanza wanakuja Dar kutoka kutoka mikoa
mbalimbali na wataishi kwa gharama zao”.
“Mgeni Rais atakuwa Naibu waziri wa Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Juma Nkamia. Pia tumemualika
mwenyekiti wa Baraza la michezo wa Taifa, Dioniz Malinzi na Rais wa TFF, Jamal
Malinzi. Wote wamethibitisha kujumuika nasi katika mkutano huo”. Bwire
amehitimisha.
0 comments:
Post a Comment