Wednesday, May 6, 2015

Baada ya kuukimbia uwanja wa CCM Kirumba kama uwanja wake wa nyumbani kufuatia vichapo mfululizo Kagera sugar sasa kurejea Mwanza.
Hayo yamewekwa bayana na meneja wa wakata miwa hao Mohammedi Hussein alipokuwa akiteta na Mpenja blog.
Mohammedi Hussein amesema, kwa mujibu wa ratiba, mchezo huo inaonesha utapigwa Mwanza na wao hawana sababu ya kuukataa uwanja huo.
"Ni kweli tutamalizia mchezo wetu hapa mwanza ambapo tumepiga kambi na ratiba inatuonesha tutacheza hapa, sisi hatuwezi kuhamisha mchezo kupeleka uwanja mwingine kwa kuwa itakuwa gharama kubwa"Alisema meneja huyo.
Mohammedi aliongeza kuwa kwa sasa timu hiyo haina cha kupoteza kwa kuwa ligi yenyewe imefika mwisho ni bora wakubaliane na matakwa ya bodi ya ligi ili wakajipange kwa msimu ujao.
"Ligi yenyewe imefika mwisho hatuna haja ya kuvutana na bodi ya ligi wala TFF, kikubwa tunamaliza mchezo wetu na tunaenda kujipanga kwa msimu ujao".Alisema.
Pia aliwaomba watu wa Mwanza kujitokeza kuishangilia timu hiyo itakapo kuwa ikimaliza mchezo wao wa mwisho dhidi ya Tanzania prisons kwenye dimba la CCM Kirumba.
Ikumbukwe Kagera iliuchagua uwanja CCM Kirumba kama uwanja wake wa nyumbani baada ya uwanja wa kaitaba kuwa katika marekebisho lakini kufuatia kupoteza michezo mitatu mfululizo dhidi ya Mbeya city, Azam fc pamoja na Ndanda timu hiyo iliamua kutimkia uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video