Wednesday, May 27, 2015

Bakari Shime

STORI kubwa jijini Tanga ni tetesi za mabingwa wa zamani wa Tanzania mwaka 1988, African Sports ‘Wana kimanumanu’ kumuwania kocha wa Mgambo JKT, Bakari Shime.
Hata hivyo kocha Shime ‘’Mchawi mweusi’ amesema kuzungumza na timu yoyote si jukumu lake kwasasa  na wanaopaswa kufanya kazi hiyo ni meneja wake Martin Kibua na wakala Nassor Binslum.
“Nimshukuru Mungu kwamba niko salama, tetesi ambazo zinasikika nimekuwa nikijibu kwa wepesi sana kwasababu mimi kama taasisi nina utawala kwa maana ya wakala, meneja na mwanasheria wangu”. Amesema Shime na kuongeza; “Mimi ninachojua vizuri sana ni kufundisha mpira, sikusomea masoko, biashara wala sheria. Wapo watu wanaozunguka na huu ndio wakati wao. Mimi nimepumzika, huu ndio wakati wao wa kufanya kazi ya kunitafutia timu na kufanya maongezi”.
“Nasikia kama anavyosikia mtu mwingine kwamba kuna African Sports, Coastal Union, Mgambo wenyewe na timu nyingine, lakini naamini ukimpata wakala wangu au meneja wangu anaweza kukwambia ukweli ni wapi wameanza mazungumzo”.
Licha ya mtandao huu kumujulisha Shime kwamba meneja wake, Martin Kibua tayari ameshasema kwamba kuna ofa mbili za Mgambo na African Sports , kocha huyo akaendelea kushikilia msimamo wake wa kufuata uweledi.
“Taarifa naweza kuwa nayo, lakini huu ndio wakati wao wa kufanya kazi, sitakiwa kuwasemea, sitakiwi kuzungumza kwa niaba yao, wakati mimi nafundisha nafanya kazi yangu, naongea na vyomvo vya habari kuhusu mambo ya ufundi, lakini wakati huu wao wanafanya kazi. Muda ukifika wataniambia kuna ofa mbili na moja tumekubaliana nayo, tutaangalia falsafa yangu na falsafa ya timu hiyo, wao wanapofanya mazungumzo wanafahamu kuwa mwalimu wetu ana falsafa gani na anaweza kufanya kazi na timu gani. Huu ni wakati wa Kibuo na Binslum kuzungumza, mimi nipo kando”. Amefafanua Shime anayeonekana kufuata uweledi katika soka.
African Sports ni timu ya wanachama tofauti na Mgambo ambayo inaongozwa na taasisi (JKT), je, Shime akienda huko ataweza kuhimili presha?
“Ni vizuri sana kwasababu mimi kama mwalimu nahitaji kupata changamoto kila wakati, huwezi kufundisha timu ambayo imelala kila wakati ukatarajia kupata mafanikio, lazima uwe na msukumo kutoka nyuma, ujue kwamba unafundisha watu wanaotaka mafanikio. Usilale usingizi, kila wakati utafute mbinu za kuwafurahisha, mimi siogopi timu ya mashabiki, siogopi timu yoyote, naamini naweza kufundisha timu yoyote” Amesema Shime.
Kwa upande wake Meneja Martin Kibua amesema kweli zipo ofa mbili kutoka kwa Mgambo wenyewe na African Sports.

“Kocha Bakari Shime ameifundisha Mgambo JKT msimu uliopita na mkataba wake unaisha mwezi huu. Magambo Shooting nao wameonesha nia ya kutaka kuendelea naye, lakini kama unavyojua ualimu ni kazi, tumepokea ofa mbalimbali, tumepata ofa ya African Sports pia. Sisi tumewapa ofa ya Mgambo ili wajitathimini. Hatujamalizana na African Sports, tupo katika mazungumzo, tunasubiri kuona ni nani ataweza kufanya kazi na Shime”

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video