Wednesday, May 27, 2015


Wakati makocha wanapofukuzwa, hasa hasa kwenye klabu kubwa, mara nyingi huwa tunaligeuza kuwa jambo la uadilifu. Tunawaonea huruma (au hapana) na huwa tunajiuliza kama walistahili kufukuzwa au walifanya kila kilichotakiwa ili kulinda vibarua vyao. Tunatumia vipimo vyetu kupima hivi – matokeo, ukubwa wa bidhaa (image), aina ya uchezaji – tunajitahidi kuwa na usawa kwa kuangalia sababu zingine zilizopunguza ubora kama: majeruhi, muda, rasilimali, uwezo wa kuongoza na maono ya mbali na mahusiano binafsi.

Mengi tuliyokwishayataja yanaingia katika uamuzi wa Real Madrid kumfukuza Carlo Ancelotti. Kwa vyovyote vile – iwe ni wachezaji au mashabiki – wengi walitaka aendelee kuwepo na waliamini juu ya kile alichokuwa anakifanya.

Kwa nini walitaka asiondoke?

Kwa wachezaji , labda sababu kubwa inaweza kuwa walipenda kufanya kazi chini yake. Aliwachukulia kama watu wazima. Alikuwa mtetezi wao kwa umma. Tofauti na wengine waliomtangulia, hakukuwa na mkanganyiko wowote iwe ni sehemu ya kufanyia mahojiano, uwanja wa  mazoezi au vyumba vya kubadililshia nguo wakati Ancelotti akiongoza.

Kwa mashabiki, itakuwa ni vile alivyoiwakilisha klabu yao, bila ya kuwapa shutuma waamuzi au klabu nyingine na kuwa mtazamo chanya muda wote, pamoja na sababu kubwa ya kuwaletea mataji manne ndani ya misimu miwili hii ikijumuisha taji lililongojewa kwa muda mrefu la Ligi ya Mabingwa. Sababu nyingine ambayo ni halisi sana, ni kuwa katika makocha wote 46 walioifundisha Real Madrid katika miaka 113 yake katika historia hakuna mwenye uwiano mkubwa wa kushinda kumzidi Carlo Ancelotti.

Lakini kanuni za kumbakiza (au kumwondoa) kocha zinabaki kuwa rahisi. Hautakiwi kuwa na huruma, kama ukiamua.

Je, kuna mtu yeyote ambaye tunadhani ataweza kufanya kazi nzuri zaidi? (inaweza kuwa kwa sababu ya matokeo, aina ya uchezaji, utambulisho, gharama au vingine)

Florentino Perez ni Rais wa Real Madrid, hiyo ndio kazi yake. Kama atafikiri mtu mwingine anaweza kufanya kazi nzuri zaidi, basi anaweza kuamua kufanya lolote.

Kitu alichofanikiwa kushinda Ancelotti (au kocha mwingine yeyote) hapo nyuma, inaweza kutumika kuona nini timu yake inaweza kushinda hapo baadae. Lakini kuna usemi usemao, “Uwezo wako wa jana, sio mafanikio ya kesho”

Florentino atazungumziwa zaidi kwenye maamuzi yake ya kumuondoa Ancelotti,na kumweka  kama ni Benitez au kocha wa Sevilla, Unai Emery au mtu mwingine. Baadae, watu watalinganisha mafanikio ya kocha atakayekuja baada ya Ancelotti. Rahisi hivyo.

Nadhani Florentino na bodi yake hapa wamechemka vibaya, na yeyote yule watakayemchagua, ukizingatia wanafanya mageuzi makubwa ya ghafla, hii itaifanya klabu kurudi nyuma. Muda utaongea.

Lakini tujikumbushe ni kwa nini Perez anafanya maamuzi kama haya kwenye moja ya vilabu vikubwa kabisa duniani. Yeye haimiliki Real Madrid;  ni mtu aliyechaguliwa kuwa Rais, uchaguzi wa hivi karibuni ni ule wa Juni 2013, alipokuwa hana mpinzani.

Kwa nini alikuwa hana mpinzani? Vizuri sababu moja inaweza kuwa, ni vizuri kwa wanachama wa Real Madrid wanapata nafasi ya kumchagua Rais ambaye ataweza kusimamia mipango yao na kila kitu, pili siku hizi uchaguzi  wao si wa kidemokrasia sana.

Mwaka 2012, bodi ya klabu (ikiongozwa na Perez) ilivipitia tena vipengele vya kusimama kugombea urais wa klabu. Aliongeza muda wa kipengele cha umri wa  uanachama kutoka miaka 15 hadi kufikia 20, lakini pia mgombea atatakiwa kuonesha kwamba ameweka benki au amepata udhamini wa benki ulio sawa na asilimia 15 ya bajeti ya mwaka. Kwa mwaka 2013, ilikuwa Dola 83 Mil; kufikia uchaguzi ujao inatarajiwa itakuwa kama Dola 120 Milioni.

Hii inamaanisha nafasi ya wagombea wengine kujitokeza kutangaza nia, inaendelea kuwa finyu. Perez ni moja ya watu matajiri sana Spain; anaendesha makampuni makubwa sana (yenye thamani ya mabilioni ya dola) ya ujenzi, akipiga mluzi tu, anajikuta amezungukwa na watu wa benki wakimwahidi udhamini wa vitu vingi. Ni ukweli usiopingika katika dunia ya leo si watu wengi wanaoweza kuiomba benki iwape udhamini wa Dola 120 Mil na huku wakiwa ni wanachama wa Real Madrid kwa miaka 20 ili waweze kugombea urais wa Real Madrid. Unaweza kuwahesabu kwa kutumia vidole vya mikono yako miwili.

Rais wa zamani kabla ya Perez, Ramon Calderon, aliwahi kutania kuwa, njia nzuri ya yeye kujihakikishia urais ni kuongeza kipengele kingine kitakachosema, wale wote ambao majina yao yanaanza na herufi “F-l-o” ndio wanaweza kugombea.

Wale wanaomsapoti Perez watasema kwamba sheria hizi hazikutengenezwa ili yeye pekee aweze kutawala Real Madrid. Bali, zinatumika ili kuilinda klabu na wale wasio na ubora, watu ambao wanaweza kuchezea hela za watu wengine katika mambo yao ya ajabu ajabu. Kama unahitaji watu maarufu na matajiri ndio wawe marais, basi hawatahitaji kuitumia Real Madrid kuwa kama chombo cha usafiri kupata utajiri.

Wakati mijadala ikiendelea, inazidi kuwa ya ajabu. Sio kwa sababu tu, urais ni zana yenye thamani kwa watu maarufu na kutengeneza mtandao hata kwa matajiri lakini sababu kubwa ni kuwa inaondoa watu wengi wenye vipaji, akili na wanaoangalia mbele kushika wadhifa huo katika klabu.

Unapokuwa katika chombo cha ndani kabisa cha uongozi na unaona kabisa kwamba kiongozi huyo anaenda kuongoza kwa muda mrefu kweli,  kwa uhalisia kabisa hii hufifiza ile hali ya mawazo kukinzana na kumpinga kiongozi huyo. Pale mambo yanapoenda mrama, basi hapo mtajichunguza wenyewe na hitimisho litakuwa lile lile kila siku: tulikuwa sahihi, hatukuwa na njia nyingine, ni bahati mbaya.

Tangu amfukuze Vicente Del Bosque mwaka 2013, Florentino amekuwa na vipindi viwili tofauti kama Rais na jumla ya makocha tofauti nane. Nini anacho cha kutuonesha? Kombe moja la La Liga na Kombe moja la Mfalme chini ya Mourinho na Kombe  moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe moja la Mfalme, Super cup moja ya UEFA na Kombe moja la klabu bingwa ya Dunia chini ya Ancelotti. Iko hivyo.

Katika taasisi ya kawaida – ile ambayo bosi mkubwa hajagundishwa kwenye kiti chake na ambayo mawazo tofauti yanakaribishwa kama chachu ya kuzidi kusonga mbele  na kufanya vema – unaweza kuhitimisha kwa kusema kuna kitu hakipo sawa hapa.


Mtazamo nao ni tatizo. Wenyewe wanadhani labda mtu mwingine anaweza kufanya vizuri katika klabu hii kuliko Ancelotti. Tutaona tu. Kitu ambacho kwa asilimia kubwa, hatutakiona – hata kama haimiliki klabu na hata kama klabu ndio inayosimamia chaguzi -- kuna mtu anaweza kufanya kazi nzuri na klabu kuliko Florentino.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video