Wednesday, May 13, 2015


Erasto Nyoni (kulia) ni miongoni wa wachezaji muhimu wa Azam fc

KAMA kuna timu ilikuwa inawakodolea macho beki wa kati wa Azam fc, Said Hussein Mourad na kiungo Erasto Edward Nyoni kitumbua kimeingia mchanga baada ya uongozi wa klabu hiyo kufanya maamuzi ya haraka.
Siku chache baada ya ligi kuu  msimu wa 2014/2015 kumalizika, Azam imekaa chini na kutafakari kwa kina, hatimaye imemuongezea mkataba wa mwaka mmoja Morad ambaye alikuwa huru toka aprili 16 mwaka huu.
Katikati ya mwezi aprili mwaka huu, Mourad kupitia mtandao huu ulitangaza kuwa huru na alikaribisha ofa kutoka timu yoyote, lakini alisema anaipa muda timu yake ya Azam kwani bado anahitaji kufanya nayo kazi.
Hatimaye mawazo yake yamekamilika na msimu ujao ataendelea kuvaa uzi wa Wanalambalamba.
Erasto Nyoni ambaye humudu kucheza nafasi ya beki na kiungo ndani ya Azam fc na Taifa Stars naye ameongezewa mkataba wa mwaka mmoja.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video