Friday, April 10, 2015


NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney yuko tayari kumpa raha kila shabiki wa Manchester United wikiendi hii timu hiyo itapochuana na watani wake wa jadi, Manchester City uwanja wa Old Trafford.
City wameshinda mechi nne mfululizo za watani wa jadi na ushindi wa karibuni zaidi ni ule wa Etihad mwezi Novemba ambao Sergio Aguero alifunga goli pekee katika ushindi wa 1-0.
Hata hivyo, Rooney amesema wana kazi kubwa kupata matokeo mazuri dhidi ya kikosi cha Manuel Pellegrini ambapo wapo nafasi ya nne katika msimamo wa ligi, pointi moja nyuma ya United wanaochuana nao jumapili.
"Tunataka kuwapa tabasamu mashabiki wa United kuamkia jumatatu asubuhi, tunataka kuwafanya wawatambie mashambiki wa Manchester City", nyota huyo mwenye miaka 29 amewaambia MUTV.
"Nadhani ni mechi muhimunkwa Manchester United na Manchester City...kwa mashabiki, kwangu mimi ni mechi ya kujichukulia nsifa kubwa".
Rooney amefunga magoli 11 dhidi ya City katika maisha yake-likiwemo boa bora la kichwa alilofunga mwaka 2011 na wikiendi hii anatarajia kuongeza rekodi yake uwanjani Old Trafford.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video