Wakati watu wengi wakiamini Jurgen Klopp anaweza
kujiunga na Manchester City baada ya kutangaza kuondoka Borussia Dortmund
mwishoni mwa msimu huu, vyanzo vya habari vinaeleza kuwa kocha huyo hatakuwepo
kwenye kinyang’anyiro cha kutua Etihad kama mabingwa hao watetezi wa ligi kuu
England wataamua kumfukuza Manuel Pellegrini.
Licha ya kocha huyo wa zamani wa Mainz kuwa na
rekodi nzuri ya kushinda mataji mawili ya Bundesliga na moja la DFB-Pokal akiwa
na Dortmund na kufika fainali ya ligi ya mabingwa mwaka 2013, Man City hawaoni
haja ya kumpa kipaumbele cha kumteua kuwa kocha wao.
Pellegrini ambaye
amebakiwa na mwaka mmoja katika mkataba wake yupo katika wakati mgumu baada ya Manchester City kupoteza mechi sita
kati ya nane walizocheza za ligi kuu pamoja na kutolewa mapema ligi ya mabingwa
barani ulaya.
Tayari Pep Gaurdiola wa
Bayern Munich anaripotiwa kuwa chaguo la kwanza kutua Etihad, lakini kocha huyo
wa zamani wa Barcelona ameweka wazi kuwa anahitaji kuendelea kufanya kazi
Allianz Arena msimu ujao

0 comments:
Post a Comment