Sunday, April 12, 2015


Wakili Dkt. Daniel Ndumbaro

SHIRIKISHO la soka Tanzania limetuma taarifa kwa vyombo vya habari jioni ya leo kuwa kamati ya rufani ya nidhamu ya Shirikisho hilo imekutana leo (Aprili 12 mwaka huu)  kujadili rufani ya Wakili Dkt. Damas Daniel Ndumbaro aliyefungiwa miaka saba na TFF kujihusisha na shughuli za soka.
Katika kikao hicho imeelezwa kuwa TFF iliwakilishwa na wakili wake Emmanuel Muga wakati Dkt. Ndumbaro hakufika wala kuwakilishwa na wakili wake, hivyo kamati chini ya mwenyekiti wake Revocatus Kuuli imeazimia kutuma wito tena kwa Ndumabaro.

Mtandao huu umemtafuta wakili maarufu Dkt. Ndumbaro kutaka kujua kwanini hakufika mbele ya kamati.

Ndumbaro amekanusha kuwa hana taarifa yoyote ya wito kutoka TFF kuhusiana na kikao cha kamati ya nidhamu.

Aidha Ndumbaro ameongeza kuwa hata alipomuuliza katibu muhtasi wake (secretary) naye amesema hajaletewa taarifa yoyote wito kutoka TFF.

“Lakini nina imani na mwenyekiti wa kamati ya rufaa ya nidhamu ambaye ni muadilifu kwa maana ya kwamba ametoa fursa ya kutuma wito mwingine kwake”. Amesema Ndumbaro na kuongeza, “Hii inaonekana wazi kuwa TFF ilipanga suala liamuriwe kwa upande mmoja , wakili wa TFF alikuwepo, lakini upande wa Utetezi wangu haukupewa taarifa yoyote juu ya kikao”.

TAARIFA ILIYOTUMWA KWA VYOMBO VYA HABARI JIONI YA LEO HII HAPA;

Kamati ya Rufaa ya Nidhamu - TFF imekutana leo tarehe 12/04/2015 kujadili rufaa No. 1/2014 ya DR. DAMAS  NDUMBARO dhidi ya TFF.


TFF iliwakilishwa na Wakili Msomi Emmanuel Muga na Dr. Ndumbaro hakufika wala hakuwakilishwa na wakili wake.


Kufuatia kutofika kwa Dr. Ndumbaro, Kamati, kwa Azimio moja, iliamuru TFF itoe wito mpya na  mpaka tarehe 14/04/2015 uwe umemfikia Dr. Ndumbaro, ukimfahamisha tarehe ya kikao kijacho cha kusikiliza rufaa yake.


Imetolewa na Mwenyekiti,

REVOCATUS KUULI

MWENYEKITI WA KAMATI


12/04/2015.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video