Ligi Kuu ya Vodacom
inatarajiwa kuendelea kutimua vumbi katika viwanja vitatu tofauti siku ya
jumatano, Mkoani Morogoro katika uwanja wa Manungu-Turiani timu ya Mtibwa Sugar
watawaribisha majirani zao timu ya Polisi Morogoro.
Katika uwanja wa
Azam Complex - Chamazi maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha maafande wenzao
timu ya Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya, huku timu ya Ruvu Shooting wakiwa
katika Uwanja wa nyumbani Mabatini - Mlandizi kuwakaribisha timu ya Ndanda FC.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
0 comments:
Post a Comment