Saturday, February 21, 2015

Na Oswald Ngonyani


Mwezi Mei mwaka 2012, Didier Drogba, aliiihama klabu yake aliyoichezea kwa mahaba makubwa klabu ya Chelsea baada ya kuichezea kwa muda wa miaka minane.


Ulikuwa uamuzi ulioonekana kuwasononesha mashabiki wengi wa ‘The Blues’ na hata baadhi yao kujikuta wakikumbwa na fadhaiko, tena fadhaiko kuu ndani ya mioyo yao.


Nakumbuka wakati akiihama Chelsea, alitajwa kuwa mchezaji bora zaidi wakati wa mechi ya fainali ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya (UEFA) ambapo Chelsea, iliibuka na ushindi dhidi ya Klabu ngumu ya Bayern Munich ya nchini Ujerumani.


Katika mchezo huo wa fainali mwanamume huyu aliyezaliwa miaka 36 iliyopita huko Abidjan nchini Ivory Coast alifunga penalti ya mwisho na kuipa Chelsea ushindi wake wa kwanza katika fainali hizo.



Baada ya kandarasi yake na Chelsea kumalizika, mchezaji huyo mwenye sifa ya kutumia nguvu zaidi dimbani aliamua kujiunga na klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki katika mechi za ligi kuu nchini Uchina.


Ripoti zinasema kuwa Drogba alijiunga na klabu hiyo baada ya kusaini mkataba wa pauni elfu mia mbili kwa wiki na tayari aliifanyia makubwa klabu hiyo kwa kuifungia magoli mara kwa mara katika kila mchezo aliokuwa amepangwa.


Umaarufu aliouonyesha Drogba, wakati wa fainali ya kombe la klabu bingwa barani Ulaya mjini Munich, Ujerumani, ulimpa heshima zaidi na wanazi wengi wa The Blues duniani kote.


Heshima kama hiyo aliipata pia barani Afrika baada ya kuiwezesha timu yake ya Taifa ya Ivory Coast kutinga mpaka katika hatua ya fainali ya AFCON 2012 lakini kwa bahati mabaya hawakuchukua ubingwa mbele ya wenyeji Zambia.


NYAKATI ZENYE MACHUNGU ZAIDI ZA DROGBA KATIKA TIMU YAKE YA TAIFA

Drogba  ambaye jina lake halisi ni Tébily Didier Yves Drogba alikiongoza kikosi hicho cha Ivory Coast kufikia fainali ya mashindano hayo kwa mara ya pili yaani mwaka 2012.


Kama ilivyokuwa katika fainali ya mashindano hayo nchini Misri, miaka nane iliyopita, fainali hiyo iliamuliwa kwa njia ya penalti. Katika mechi hiyo, Zambia ambayo haikutarajiwa na wengi kushinda, ilivunja ndoto ya Drogba ya kushinda kombe hilo na timu yake ya taifa.


Kwa Drogba hilo lilikuwa pigo kubwa mno na kamwe hatakuja kulisahau asilani. Katika nyakati zake zote za Unahodha wa Timu ya Taifa hajapata bahati ya kutwaa ubingwa huo, katika awamu tofauti alionekana kujidhatiti sana kwa dhati ya moyo wake lakini alishindwa kabisa kukidhi haja ya uhitaji wake.


KUHUSU UFALME WAKE PALE DARAJANI


Wakati alipokuwa akiichezea Chelsea hususan katika misimu ya mwaka 2004 mpaka mwaka 2012 Drogba alifunga zaidi ya magoli 150 na kucheza takriban mechi 350. Alishinda kombe la ligi kuu ya Premier mara tatu, kombe la FA mara nne na kombe la ligi mara mbili.


Mwezi Oktoba mwaka 2012 mashabiki wa Chelsea walipiga kura ambapo aliibuka kuwa mchezaji bora zaidi kuwahi kusajiliwa na klabu hiyo tangu ilipoanzishwa.



Drogba aliwahi kushinda taji la BBC la mchezaji bora barani Afrika mwaka wa 2009 na licha ya kukumbwa na maswaibu katika maisha yake, Drogba hakupoteza muda na nafasi aliyopata alijikakamua na kuwa mmoja wa wachezaji bora zaidi kutoka Afrika.


Kujituma kwake ndani ya dimba kumemfanya aheshimike zaidi katika mawanda ya soka la England lakini pia katika mawanda ya soka la Afrika na  duniani kwa ujumla.


ALIVYOPOKELEWA KWA MIKONO MIWILI STAMFORD BRIDGE NA MWALIMU WAKE KIPENZI JOSE MOURINHO


Pamoja na maisha ya soka kumuendea vema sana nchini China, Ujio wa Kocha wake wa zamani, Kipenzi chake Jose Mourinho pale darajani ulimfanya arudi tena kucheza Ligi kuu ya England EPL huku akipewa nafasi zaidi na Kocha wake huyo, nafasi ambayo mpaka sasa ameonekana kuitendea haki na hata kuwaridhsisha mashabiki wake.


Ukongwe wa umri wake ulionekana kuwatisha mashabiki wengi wa Chelsea, lakini Jose Mourinho alionekana kuona mbali zaidi na kuwataka mashabiki hao kutokuwa na hofu kuhusu Drogba.

Hata yeye Drogba alionekana kuridhishwa sana na uamuzi wake wa kurudi katika klabu yake ya zamani, klabu aliyoitumikia kwa mahaba makubwa kuliko.


Nakumbuka mara baada ya kusaini mkataba wake wa mwaka mmoja wa kuitumikia klabu hiyo alizungumza maneno machache yaliyokuwa na maana kubwa sanaa:


“Yalikuwa maamuzi rahisi nisingeweza kupoteza nafasi ya kufanya kazi tena na Jose. Kila mtu anajua mahusiano mazuri niliyokuwa nayo na klabu hii, na mara zote nimekuwa nikijisikia kama nyumbani”. 


“Hamu yangu bado ni ile ile na naangalia mbele kuisaidia timu hii. Namefurahia sana ukurasa huu mwingine wa maisha yangu ya soka”.


Naye Mourinho aliwaondoa hofu mashabiki wa klabu hiyo akisisitiza kuwa Muivorycost huyo bado ni mshambuliaji bora katika ulimwengu wa soka.


“Amekuja kwa sababu ni miongoni mwa washambuliaji bora Ulaya. Namjua sana na najua kuja kwake kutamfanya ayafanye yale makubwa aliyowahi kuyafanya klabuni miaka ya nyuma”, Alisema Mourinho.



Drogba ambaye katika fainali za sasa za AFCON 2015 hakuwepo katika kikosi cha Taifa cha Ivory Coast baada ya kustaafu aliiangalia timu yake kupitia Televisheni ambapo Tembo hao wanaoongozwa na mchezaji bora wa Afrika, kiungo Yaya Toure walifanikiwa kuutwaa ubingwa wa AFCON, ubingwa ambao walikuwa wameumisi sana.


Atakumbukwa kutokana na uwezo wake ndani ya dimba, uwezo ambao kwa kiasi kikubwa uliiwezesha timu yake ya Taifa kucheza fainali ya AFCON katika awamu mbili tofauti lakini pia uwezo wake huo kwa kiasi kikubwa ulichagiza timu yake ya Chelsea kufanya vema katika mashindano ya ndani na nje ya England.


Naomba kutamatisha.


Unapenda kuwa Mkufunzi wa mchezo wa soka? Nunua sasa Kitabu cha ‘SIRI YA SOKA’ Uweze kuwa na uelewa zaidi katika mchezo huo, Wasiliana na Mwandishi wa Makala haya kwa  simu namba 0767 57 32 87 ili kuweza kujipatia nakala ya Kitabu hicho.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video