
Kazi kwisha: Wachezaji wa Albania wakishangilia baada ya kuilaza Ureno katika mchezo wa kuwania kucheza Euro 2016
URENO ikiwa bila nyota wake Cristiano Ronaldo imechapwa bao 1-0 katika uwanja wa nyumbani dhidi ya Albania katika mchezo wa ufunguzi wa kuwania kufuzu fainali za Euro 2016.
Baada ya kufanya vibaya kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil, Ureno jana usiku walishindwa kusawazisha bao la dakika za mapema kipindi cha pili lililofungwa na Bekim Balaj.
Hata kama Ronaldo hakuwepo, Fabio Coentrao na Nani - waliongoza timu ya Ureno katika mchezo huo wa kundi I, lakini walishindwa kujibu mapigo.
Nani aliyesajiliwa kwa mkopo na Sporting Libson kutokea klabu ya Manchester United alipiga krosi nyingi za hatari, lakini washambuliaji wenzake walishindwa kuzibadili kuwa magoli.

Mshituko: Mshambuliaji wa Albania, Bekim Balaj (katikati) akishangilia baada ya kufanga bao la kuongoza dhidi ya Ureno mjini Aveiro

Kitu cha ukweli: Bekim Balaj akifunga goli la kuongoza
0 comments:
Post a Comment