Thursday, August 7, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


Imechapishwa Agosti 7, 2014, saa 5:11 asubuhi

MAGWIJI wa Real Madrid maarufu kama ‘Real Madrid Legends’ wanatarajia kufanya ziara nchini Tanzania kuanzia Agosti 22 mwaka huu ambapo watacheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya kikosi maalumu cha nyota wa Tanzania Agosti 23 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kiingilio cha chini katika mechi hiyo ya kihistoria kitakuwa  buku tano tu (5,000) na lengo ni kuwapa fursa Watanzania wengi kuwaona Magwiji wa Bernabeu waliowahi kutamba katika michuano ya La Liga, UEFA na kombe la dunia wakiwa na nchi zao.

Kwa mujibu wa meneja wa ziara hiyo, Dennis Ssebo, wachezaji mbalimbali wameshathibitisha kuwasili Tanzania na maandalizi kwa ujumla yanakwenda barabara.

Mtandao huu kuanzia leo utakuwa unaangazia historia fupi ya magwiji wote watakaokuja nchini, yaani kuanzia wa kwanza mpaka wa mwisho na leo hii tunaanza na:

1.   PEDRO CONTRERAS GONZÁLEZ-

Huyu ni kipa mstaafu wa Hispania. Alizaliwa mwaka Januari 7, 1972 mjini Madrid. Urefu wake ni futi 5 na inchi 11.

Kipa huyo alicheza mechi 246 za La Liga katika misimu 13 aliyokaa langoni. Alizichezea klabu za Real Madrid, Rayo Vallecano, Malaga na Betis na kumalizia soka lake katika klabu ya Cadiz CF, msimu wa 2007-08.

Katika fainali za kombe la dunia mwaka 2002 ambapo Brazil chini ya kocha Luis Felipe Scolari walitwaa kombe nchini Korea kusini na Japan, Contreras aliichezea timu yake ya taifa ya Hispania kwa mara ya kwanza na ya mwisho.

Hili ni zao la Real Madrid katika mfumo wake wa soka la vijana. Kipa huyu aliyezaliwa mjini Madrid, alivaa medali ya UEFA mwaka 1998, lakini hakucheza hata dakika moja katika msimu huo.

Alikaa miaka minne na kikosi B, Real Madrid Castilla na alionekana katika michezo minne ya timu ya kwanza msimu wa 1998-99 ambapo Real Madrid ilimaliza katika nafasi ya pili.

1996-97 alitolewa kwa mkopo kwenda klabu ya Rayo Vallecano ambapo alikosa mechi moja tu ya ligi kuu katika mechi 42.

Contreras alijiunga na Malaga FC katika msimu wa 1999-2000. Alikuwa kipa chaguo la kwanza ambapo alikosa mechi sita tu kutoka 1999-2003.

Kipa huyo alijiunga na Real Betis mwaka 2003, ambapo alicheza mechi 22 za ligi kuu katika msimu wa 2003-04, na nyingine alizikosa baada ya kupata majeruhi na kumpisha Toni Doblas.

Msimu wa 2005-06 alishindani katika makombe ya UEFA na ligi ya mabingwa ampapo hakufungwa bao katika mechi mbili dhidi ya Chelsea katika ushindi wa 1-0 hatua ya makundi.

Alitolewa kwa mkopo Cadiz CF msimu wa 2007-08 akicheza sambamba na Dani. Contreras aliachwa baada ya msimu kumalizika. Baada ya hapo alistaafu soka na kujiunga na klabu yake ya zamani ya Malaga kama kocha wa makipa.

MAKOMBE ALIYOSHINDA

Real Madrid

·         UEFA Champions League1997–98

·         Intercontinental Cup1998

·         La Liga1994–95

·         Supercopa de España1997

Málaga

·         UEFA Intertoto Cup2002

Betis

·         Copa del Rey2004–05



Kesho tutakuletea historia ya gwiji mwingine atakayetua Tanzania, Agosti 22 mwaka huu, ni nani huyo? tafadhali endelea kutufuatilia….

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video