Monday, August 4, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976


Imechapishwa Agosti 4, 2014, saa 5:22 asubuhi

MPIRA wa miguu ni mchezo wa mipango, huwa hauna njia ya mkato ili kufikia kilele cha mafanikio.

Mataifa yote yaliyofanikiwa na yanayoendelea kufanikiwa katika mchezo wa soka ni kutokana na uwekezaji mkubwa na mipango thabiti hasa katika soka la vijana.

Nchi kama Ujerumani, imelitengeneza soka lake kwa zaidi ya miaka 10 mpaka kufikia mafanikio ya kutwaa ubingwa wa kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil.

Ujerumani imetengeneza mfumo sahihi wa soka la vijana, kila timu inayoshiriki ligi kuu nchini humo, Bundesliga ina timu bora ya vijana wa umri toafuti, walimu wenye taaluma za juu na akademi za uhakika.

Vijana wengi wanazalishwa kwa ajili ya kutumika katika timu za wakubwa kwa baadaye. Timu zina malengo ya muda mrefu.

Hali hii inasababisha urahisi kuunda timu ya Taifa ya vijana ya Ujerumani, na ndio maana juzi juzi tu wamelitishia soka la dunia baada ya timu ya Taifa ya chini ya miaka 19 kutwaa ubingwa wa kombe la Ulaya kwa vijana.

Kaka zao wametoka kutwaa kombe la dunia kwa mipango sahihi, madogo nao wanafuata nyayo zao. Hakika mpira ni mpango na sio njia ya mkato ‘shortcut’.

Hata ukifuatilia Hispania, wametawala kwa muda mrefu katika soka la dunia kwasababu ya uwezaji mkubwa walioufanya katika soka la ndani. Pia Uholanzi wana Historia ya kuwa na mipango mizito katika soka la vijana.

Nchi kama Cost Rica, Colombia, Uruguay, Korea Kusini, Iran zimejitahidi kusogea mpaka kufika pale zilipo kutokana na uwezezaji na mipango sahihi.

Afrika magharibu imetawala soka la Afrika kwa muda mrefu kwasababu ya uwezezaji mkubwa walioweka pamoja na kujali soka la vijana.

Jana Tanzania imetolewa na Msumbiji katika michuano ya kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika, mwakani nchini Morocco.


Stars ilitoka sare ya 2-2 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam wiki mbili zilizopita na jana ilifungwa mabao 2-1 katika uwanja wa Taifa wa Zimpeto, nje kidogo ya Mji wa Maputo, hivyo kutolewa kwa wastani wa mabao 4-3.

Baada ya mechi hiyo, nimefuatilia mijadala mingi ya watu wa mpira. Kila mtu anasababu zake na maoni yake. Wapo wanalilaumu benchi la ufundi chini ya kocha mkuu Mart Nooij, wengi uongozi wa TFF na wengine wanawabebesha lawama zote wachezaji.

Walio wengi wanalaumu kuwa wachezaji wa Tanzania kwa asilimia zote ni wabovu, sio wazalendo na hawana malengo na nchi yao.

Kiufupi! lawama zote zinaweza kuwa sahihi kwasababu yanapotea makosa , lazima wa kulaumiwa awepo. Wachezaji wanabeba msalaba kwasababu wao ndio wanaocheza mpira wakati wengine ni mashabiki tu.

Kimsingi, tatizo kwa soka letu lipo. Kabla ya mechi ya jana, jumamosi timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys ilifungwa mabao 4-0 na Afika kusini ‘Amajimbos’ na kutupwa nje ya michuano ya kufuzu fainali za vijana.

Rais wa TFF, Jamal Malinzi alishuhudia mechi hiyo na baada ya mechi alikiri wazi kuwa tatizo la timu zetu ni maandalizi mabovu yatokanayo na uwezo mdogo wa kiuchumi pamoja na kukosekana kwa mfumo sahihi wa soka la vijana.

Malinzi aliongea vitu mbalimbali, lakini niliona ana hoja kubwa katika mpango wa soka la vijana. Alisema wapo kuandaa mpango maalumu wa kitaifa wa soka la vijana ili kupata muendelezo mzuri wa soka la vijana na hatimaye timu ya taifa ya wakubwa.

Hakuna jinsi ya kuchomoka hapa tulipo bila Taifa kukubali kukaa chini na kuangalia mfumo wake wa soka la vijana na hatimaye kutafuta njia ya kuboresha zaidi.

Soka la vijana litatusaidia. Kuna haja ya kuwa na akademi zitakazowalea wachezaji wetu kuanzia miaka 10-12, 12-14, 14-16, 16-18, 18-21 na hatimaye timu ya wakubwa.

Mchezaji mzuri wa miaka 10-12 anapofikisha miaka 14, anatakiwa kuhamia daraja la 14-16 na kuendelea kadiri miaka inavyozidi kukatika.

Manake kama mchezaji ataendelea kubakia katika kiwango chake, anaweza kujikuta amefika timu ya wakubwa akiwa ameshacheza timu zaidi ya tatu za Taifa za vijana. Hii itakuwa faida kubwa.

Pia itawafanya wachezaji kujijenga kiuchezaji na kuwa wazalendo kwa nchi. Itakuwa rahisi kupata timu ya taifa imara.

Tutalaamu , tutatukana, lakini mwisho wa siku, viongozi na wadau wa soka, hawawezi kukwepa kurudi katika soka la vijana kama wanataka kufika Morocco.

Mimi siamini kama tutakuja kufanikiwa bila kurudi nyuma zaidi. Tutaendelea kutiana moyo na kuombeana dua,  wakati nao maadui zetu wanaomba Mungu huyo huyo.

Unadhani Mungu atamsaidia nani kati ya aliyejiandaa vizuri na akamuomba na yule aliyejiandaa kwa tia maji tia maji kama sisi?

Tutaona Mungu anawapendelea wenzetu na kuona hana maana kwetu, kumbe wachawi wa soka letu ni sisi wenyewe. Mwisho wa siku tutakufuru kwa madai ya Mungu kutusahau Watanzania. Mungu habariki penye sifuri.

Asubuhi njema kwa wote!



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video