Wachezaji wa Coastal Union wakiwa mazoezini uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Imechapishwa Agosti 17, 2014, saa 6:43 mchana
WAGOSI wa Kaya, Coastal Union wenye makazi yao
jijini Tanga, ‘Waja leo waondoka leo’ wanaendelea kujiwinda na msimu mpya wa
ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kushika kasi septemba 20 mwaka
huu.
Kocha mkuu wa klabu hiyo, Mkenya, Yusuf Chipo
amesema tatizo linalofanyiwa kazi kwasasa ni safu butu ya ushambuliaji, hivyo
wanafanya usajili makini kuhakikisha wanaiboresha.
“Tatizo la Costal Union kwa siku nyingi ni safu ya
ushambulizi na katika usajili wetu tumekuwa tukitilia mkazo sehemu hii ya
mbele. Tunatafuta wachezaji wazuri wenye uzoefu, na nadhani kwasasa tumepata
jawabu letu” Alisema Chipo.
“Baada ya kusajili. Kilichobaki sasa ni
kuwafanyisha watu mazoezi ili waelewane, watu waingiane na tumalizie usajili”
Hata hivyo, Chipo alisema ili kujipanga zaidi
wanahitaji kuweka kambi ya maandalizi kisiwani Pemba.
“Tuna mipango ya maandalizi, tunataka kucheza
mechi za kirafiki. Kuna safari tunaandaa ya kwenda Pemba ambapo tutakaa kwa
wiki tatu au nne kwa ajili ya maandalizi’. Alisema Chipo.

Coastal Union watakutana na Yanga sc ambao
wanatarajia kuelekea Pemba wiki ijayo kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya ligi
kuu bara.
Kocha mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo
alipendekeza kambi kuwekwa Pemba ili kuwapa wachezaji wake mazoezi katika hali
ya utulivu.
Wakati huo huo, Wekundu wa Msimbazi Simba
wamejificha kisiwani Unguja wakijiwinda na msimu mpya wa ligi kuu.
Kocha mpya wa Simba sc, Mzambia, Patrick Phiri
amesifu mazingira ya Zanzibar na kusema yatamfanya ajipange vizuri na kampeni
za kuusaka ubingwa wa ligi kuu bara.

.jpg)
0 comments:
Post a Comment