Monday, August 18, 2014

Rwanda Football Federation
RWANDA itakata rufaa dhidi ya maamuzi ya kuwaondoa kushiriki hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika baada ya kumtumia mchezaji asiyekuwa na sifa.

Shirikisho la nchi hiyo limethibitisha kuwa lipo tayari kukata rufaa na litaipeleka kesi hiyo katika mahakama ya juu ya rufani ya michezo kama maamuzi hayo hayatafutwa.

Rwanda iliondolewa katika  mashindano jumamosi na kamati ya mashindano ya shirikisho la soka barani Afrika CAF.

Hatua hiyo inafuatia malalamiko kutoka kwa shirikisho la soka la Jamhuri ya Congo kuwa Rwanda ilimtumia mchezaji Birori Dady ambaye hati zake za kuzaliwa ni tofauti na zile zilizowasilishwa kabla ya mechi ya mchujo wa kombe la mabingwa barani Afrika dhidi ya DRC mwezi uliopita huko Pointe-Noir.
Shirikisho la Congo lilidai kuwa mchezaji huyo, Birori Dady  anayeichezea AS Vita anatumia hati ya Congo yenye jina la Etekiama Agiti Tady.
CAF walizifanyia uchunguzi nyaraka zilizotolewa na mashirikisho ya Rwanda, Congo na DR Congo na pia walimhoji mchezaji Agosti 11 makao makuu ya CAF mjini Cairo, Misri.

Wakati Rwanda wanaendelea kushikilia msimamo kuwa mchezaji Dady  Birori ana hati moja ya utambulisho wa uraia, uchunguzu unaonesha kuwa alitumia jina la Etekiama Agiti Tady wakati wa kujiunga na timu ya taifa.

Mchezaji aliyeigharimu Rwanda
CAF alisimamia ukweli kwamba mchezaji ana hati mbili zenye majina mawili na umri tofauti na kusema hati hizo zinamhusu mtu mmoja.
Baada ya hapo, Shirikisho hilo lilitangaza kumsimamisha mchezaji mpaka hapo watakapotoa taarifa zaidi na kumfungia kuichezea klabu yake na timu ya taifa ya Rwanda.

Rwanda iliitoa Congo kwa mikwaju ya penalty baada ya mechi mbili na kufuzu hatua ya makundi, lakini sasa timu iliyofungwa ndio imefuzu kwenda kundi A la kuwania kufuzu fainali za AFCON nchini Morocco 2015 ambapo itakutana na Nigeria, Sudan Na Afrika kusini.

Hata hivyo CAF imesema itatoa maamuzi zaidi kama itaongeza adhabu baada ya kikao cha kamati ya mashindano kitakachofanyika Septemba 17 mwaka huu.


CAF imetoa wito kwa wachezaji na wadau wa soka kuwa makini na uraia wa nchi mbili.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video