
Aliaga kwa machozi: Tunu ya Chelsea , Frank Lampard atajiunga na Manchester City kwa mkopo.
Imechapishwa Agosti 3, 2014, saa 7:22 mchana
MANUEL Pellegrini amethibitisha kuwa Frank Lampard jumatano ijayo ataanza mazoezi na Manchester City kwenye uwanja wa Carrington na atakuwa mchezaji muhimu kwenye mechi za ligi kuu na ligi ya mabingwa mpaka atakapoondoka kwenda Marekani mwezi januari mwakani.
City wamewasili nyumbani kutoka Marekana leo jumapili baada ya kupoteza nafasi ya kucheza fainali ya michuano ya kimataifa ya kujiandaa na msimu kwa mikwaju ya penalti.
Katika siku nne, City wamepoteza mechi mbili kwa penalti.
Baada ya mechi, Pellegrini kwa mara ya kwanza alizungumzia kumsajili Frank kwa mkopo na kusema maamuzi ya kumchukua kiungo huyo wa kimataifa wa England mwenye miaka 36 ni kumfanya awe fiti kabla ya kuanza kuichezea klabu yake ya New York City mwakani.

Lampard alijiunga na New York City akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Chelsea.
Pellegrini alisema: 'Kuanzia jumatano ijayo ataanza kufanya kazi na timu na atacheza mpaka januari na tutaona baada ya hapo'.
'Kwa wakati huu atafanya kazi na kikosi na atakuwa mmoja wa wachezaji wa kikosi. Atapambana kusaka nafasi'
'Anajua tuna timu nzuri, tuna wachezaji wengi katika nafasi yake na yeye ameongezeka. Tuna mechi nyingi sana hususani za ligi ya mabingwa, kwahiyo ni mtu muhimu sana kwa timu'
0 comments:
Post a Comment