Usajili: Radamel Falcao alijiunga na Monaco majira ya kiangazi mwaka jana baada ya kucheza kwa mafanikio katika klabu ya Atletico Madrid.
RADAMEL Falcao bado anazivutia klabu za England ikiwemo Liverpool, ingawa mchezaji mwenyeye ana matumaini ya kujiunga na Real Madrid.
Mshambuliaji huyu wa Colombia, ambaye mwaka jana alijiunga na Monaco ya Ufaransa kwa dau la paundi milioni 50 kutokea klabu ya Atletico Madrid anaonekana kutoridhishwa na ligi ya Ufaransa na anatamani kurudi Madrid.
Majira haya ya kiangazi tayari Real Madrid wametumia paundi milioni 90 kuwasajili James Rodriguez, Toni Kroos na Keylor Navas na sasa wanajipanga kutovunja sheria ya matumizi ya fedha ya UEFA.
Liverpool wanataka kumchukua Falcao kwa mkopo kwa malengo ya kumsajili moja kwa moja msimu ujao, lakini Monaco hawataweza kukubaliana na masharti hayo wakati wanaamini Real Madrid wataweza kulipa dau zuri.
La Liga: Real Madrid wanaiwania saini ya Radamel Falcao.

0 comments:
Post a Comment