
Na Mwandishi Wetu, Tanga
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union
ya Tanga umeizidi kete klabu ya
Simba
SC baada ya kumsajili kiungo kati wa timu ya Gormahia ya nchini
Kenya,Rama
Saluma Mohamed aliyekuwa akiwaniwa na klabu hiyo.
Rama
ametua kwenye klabu ya Coastal Union akitokea nchini Kenya
na
kusaini mkataba wa kuitumikia timu hiyo kwa kipindi cha mwaka
mmoja.
Rama
aliyewahi kuicheza timu hiyo kwa mafanikio makubwa na kufanikiwa
kupata
namba kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya Harembee Stars
alitua
jijini Tanga juzi usiku akiwa na kulakiwa na viongozi wa klabu
hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye
makao makuu ya Klabu
hiyo
barabara 11,Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi amesema kikosi
cha cha timu hiyo msimu ujao kinatarajiwa kuwa tishio kutokana na
kufanya usajili wa nguvu ambao unaonekana utaleta upinzani
mkubwa sana.
Aidha
amesema kikosi chetu msimu ujao kitakuwa tishio kwa
sababu
tunamatumaini makubwa ya kufanya vizuri kutokana na usajili imara
ambao tumeufanya kwa kusajlili wachezaji nyota kama vile Obina,Shabani
Kado Sued Tumba ,Bakari Mtama, na wengine wengi walipo kwenye
kikosi cha timu hiyo
Amesema
bado wanaendelea na mchakato wa kuhakikisha wanaimarisha kikosi
hicho kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa ligi kuu
Tanzania bara msimu ujao.

0 comments:
Post a Comment