Tuesday, August 5, 2014

Na Mwandishi Wetu, Tanga

Imechapishwa Agosti 5, 2014, saa 7:00 mchana

TIMU ya Coastal Union ya Tanga inatarajia kucheza mechi mbili za kirafiki katikati ya wiki hii ambazo zitachezwa kwa nyakati tofauti ikiwa ni maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa Ligi kuu soka Tanzania bara inayotarajiwa kuanza mwezi Septemba mwaka huu. 
Akizungumza jana, Meneja wa timu ya Coastal Union, Akida Machai alisema mechi hizo zitachezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga ambapo ya kwanza itachezwa Kesho(leo) kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani. 
Machai alisema mechi hiyo itakuwa dhidi ya Muheza Shooting na maandalizi ya kuelekea mchezo huo yamekamilika kwa asilimia mia moja na kinachosubiriwa ni siku ya mechi hiyo.

 Alisema mechi ya pili itachezwa Ijumaa wiki hii dhidi ya AFC ya Arusha kwenye uwanja wa Mkwakwani lengo likiwa kukipa makali kikosi hicho cha ligi kuu soka Tanzania bara. 
    “Kama nilivyosema mechi hizi zote ni muhimu sana kwa kila timu ambapo baada ya kumalizika uongozi utaangalia ni timu gani ya kwenda kucheza nayo “Alisema Machai. 

Hata hivyo aliwataka wapenzi na wanachama kujitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo huo ambao unatazamiwa kuwa na ushindani mkubwa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video