Wednesday, July 2, 2014



 http://ptblog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2014/04/DSCN1347-FILEminimizer.jpg
Mkenya, Tom Alex Olaba anaendelea na mkakati wake wa kusuka kikosi chake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kushika kasi mwezi agosti mwaka huu.

Na Frank Momanyi, Dar es salaam

Imechapishwa Julai 2, 2014, saa 9:16 alasiri

BAADA ya kuingia kambini mapema kabisa, klabu ya wapiga kwata wa Ruvu Shooting yenye maskani yake mabatini, Mlandizi,  mkoani Pwani imeendelea kujiimarisha kwa kufanya usajili wa wachezaji wapya kwa mujibu wa mapendekezo ya kocha mkuu, Mkenya, Tom Alex Olaba.
Afisa habari kwa klabu hiyo, mwenye maneno mengi, Masau Bwire ameiambia MPENJA BLOG kuwa klabu hiyo imefanikiwa kuwanasa wanandinga watano wenye uzoefu wa hali ya juu katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara kwa lengo la kumaliza katika nafasi nzuri msimu ujao.
Masau alisema klabu hiyo inafuata taratibu zote za uongozi na haifanyi mambo kiholelaholela kama zinavyofanya klabu zingine zinazoshiriki ligi kuu hususani Simba na Yanga.
“Sisi huwa tunafanya kazi kutokana na maelekezo ya mwalimu. Kila mmoja aheshimu kazi ya mwenzake na hapo tutaweza kusonga”. Alisema Masau.
 “Mpaka sasa tumeshasajili wachezaji watano wenye uzoefu na ligi kuu ambao kocha Tom Alex Olaba aliwapendekeza. Wachezaji hao ni pamoja na Zuberi Dabi kutoka kagera sugar,Salvatory Ntebe,Juma Mpakala na Yusuf Nguya wote kutoka mtibwa sugar ambao mikataba yao imemalizika,  bila kumsahau Muzinga ambaye alikuwa anakipiga katika ligi ya nchini Burundi” aliongeza Masau Bwire.
Maafande wa Ruvu shooting walifanikiwa kumaliza nafasi ya  sita katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita nyuma ya vinara wa ligi, Azam fc, Yanga, Mbeya city, Simba sc pamoja na wanankulukumbi kagera sugar.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video