
Hakuna njia ya kupita: Tim Howard akimnyima mchezaji mwenzake wa Everton ambaye anaichezea Ubelgiji, Kevin Mirallas kufunga bao kipindi cha pili.
MAREKANI
imetupwa nje ya kombe la dunia baada ya kuchapwa mabao 2-1 dhidi ya
Ubelgiji katika mchezo wa 16, lakini mlinda mlango wako, Tim Howard
ameweka rekodi mpya ya kombe hilo baada ya kuokoa michomo ya hatari 15.
Howard
ndiye aliwapeleka wapinzani wao, Ubelgiji, kufika dakika 30 za nyongeza
baada ya dakika tisini kumalizika kwa suluhu ya bila kufungana, lakini
katika dakika hizo, Howard alikuwa shujaa kwa kuokoa michono mingi
golini kwako.
Kijana wa kazi: Howard aliokoa michomo mingi zaidi ukilinganisha na kipa mwenzake wa Ubelgiji, Thibaut Courtois
Howard akijitanua na kuokoa mpira uliopigwa na nahodha wa Ubelgiji Vincent Kompany
Kwa kuokoa michomo 15, kipa huyo wa Everton ameandika rekodi mpya ya kombe la dunia tangu takwimu kama hizo zipatikane mwaka 1966 ambapo kipa wa Peru, Ramon
Quiroga aliokoa michomo 13 mwaka 1978 dhidi ya Uholanzi.
Kiwango cha jana cha Howard ndio bora zaidi kuwahi kutokea katika timu ya Marekani tangu Sylvester Stallone afanye hivyo mwaka 1981.
0 comments:
Post a Comment